Thursday 8 August 2013

KUELEKEA KINDUMBWENDUMBWE CHA LIGI KUU YA SOKA YA ENGLAND.



Sakata la Luis Suarez kutaka kuikacha Liverpool kuelekea Asernal;

·     Bosi wa Liverpool Brendan Rodgers, amtaka Suarez kujikosoa



·     Asema Suarez ameonesha dharau kubwa licha ya kupewa kila kitu na klabu hiyo.

        Na. deo kaji makomba.

Mshambuliaji wa timu ya soka ya Liverpool, Luis Suarez, ametakiwa na bosi wa klabu hiyo, Brendan Rodgers kujikosoa na kujifunza yeye mwenyewe, na kuongeza kuwa Suarez ameonesha dharau kubwa kwa majogoo hao wa Anfeld.

Rodgers pia amepinga madai ya mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Uruguay  ya kwamba aliahidiwa ataondoka ndani ya klabu hiyo katika msimu huu wa kiangazi endapo kama Liverpool haitashinda katika ligi ya mabingwa barani ulaya.

Suarez mwenye umri wa miaka 26, yuko katika mpango wa kuwasilisha maombi yake ya uhamisho wiki hii kama mchakato wake wa kuelekea kwa washika bunduki wa London, Asernal the Gunners, utazuiliwa na uongozi wa Liverpool.

“Hakukuwa na ahadi yoyote iliyotolewa na hakuna ahadi iliyovunjwa.” Alisisitiza Rodgers.
“Klabu na mwakilishi wa mchezaji huyo, wamekuwa na mazungumzo na alijua sahihi wapi alikuwa.
“Amekuwa dharau ya hali ya juu kwa klabu, klabu ambayo ilimpatia mchezaji huyo kila kitu.” Alisema bosi huyo wa Liverpool.

No comments:

Post a Comment