Thursday 6 February 2014

KUELEKEA KOMBE LA DUNIA NCHINI BRAZIL 2014 MAANDALIZI YA VIWANJA YAENDELEA KUKAMILIKA

Na. Josephat Kaira.


Kama kawaida yetu kisima cha burudani kinaendelea kukupatia mambo mazuri kuhusiana na burudani kitaifa na kimataifa ,zikiwa zimesalia siku chache kabla ya kuanza kivumbi  cha soka cha kombe la dunia kwa mwaka 2014 nchini brazil kitakacho shirikisha timu 32 tumeona ni vizuri tukaanza kukufahamisha viwanja ambavyo vitakuwa vikitumika katika michuano hiyo mikubwa.
Arena de sao  Paulo

Uwanja wa kwanza ni  arena de sao  Paulo,huu ni uwanja ambao uko mjini kabisa katika jiji la sao Paulo hili ni jiji maarufu na lenye idadi kubwa ya watu na linategemewa kubeba idadi kubwa ya mashabiki kutoka kona mbalimbali za dunia  unachukua idadi ya watu  65,807 unamaliziwa vizuri mwezi huu wa februari na cha kukuongezea ni kuwa wakati wa matengnezo yake hivi karibuni uliua wajenzi wawili katika ajali iliyotokea wakati wa ujenzi wa uwanja huo novemba 27 mwaka jana.

Uwanja mwingine utakaotumika katika kipute hicho ha kombe la dunia mwaka 2014 nchini brazil ni estadio mineirao bero herizonte huu ni miongoni mwa viwanjab vikongwe vya soka nchini brazil ulijengwa mwaka 1965 lakini ukafanyiwa ukarabati mkubwa mwaka 2013 lengo likiwa ni kuuweka sawa kabla ya michuano hiyo  kuanza,unachukua mashabiki  62,547 uko miles kutoka rio de geneiro.
 Estadio mineirao bero herizonte

Tukiwa tunendelea kuahamishana viwanja vingine ambavyo vitkuwa vikitumika katika michuano ya kombe la dunia kwa mwaka huu wa 2014 baada ya hivyo viwili vya hapo juu estadio costelao Fortaleza huu ulianza kutumika mwaka 1973 ukafanyiwa ukarabati mkubwa mwaka 2013 unabeba mashabiki wapatao 64,846.
 Estadio costelao Fortaleza

Uwanja  mwingine ni estadio maracana rio de janairo huu ni uwanja mwingine baab kubwa ambao nchi ya brazil itakuwa ikijisifia katika michuano hiyo huko jijini rio de janairo kwa watoto wa mujini vilevile unavikolombezo vingi pia unabeba mashabiki wengi wapatao 76,804 kuzidi ata viwanja vingine tulivyotangulia kukuelezea apo awali.
 Estadio-maracana

Estadio nacional brasilia  huu unachukua mashabiki 68,009 ulifunguliwa mwaka 1974 ila ukaanyiwa tena ukarabati mwaka 2013 mwezi may.
 Estadio-Nacional-de-Brasilia-Julio-Cecilio

Kwa leo tutahitimisha na kukufamisha uwanja wa  arena pernambuco recife huu ni uwanja mpya kabisa ukijengwa hivi karibuni na kufunguliwa mwaka 2013 mwezi may na unachukua mashabiki wapatao 44,248 ni moja kati ya viwanja vitakavyo nogesha michuano hiyo kwani kwa nje kina muwako muwako furani wa kupendeza.


Arena pernambuco recife usiku

Naam kwa wewe unae endelea  kutufuatilia wana kisima cha burudani tutakutajia viwanja vingine vitakavyotumika katika kipute cha kombe la dunia mwaka huu nchini  brazil kadri tuwezavyo endelea kuwa nasi.

Naye mshambuliaji dimitar berbatov amebainisha kuwa mlinzi wa Manchester united mfaransa Patrice evra ndiye aliyemshawishi kujiunga na club ya Monaco katika kipindi cha usajili cha mwezi uliopita wa januari.

  Berbatov

Berbatov raia wa burigaria amesema kuwa rafiki yake evra waliyekuwa wakicheza wote Manchester united kati ya mwaka 2008 hadi 2012 ndiye aliyemwambia mambo mazuri yaliyopo Monaco na kumshawishi kujiunga nayo kwa mkopo akiziba pengo la mkolombia radamel falcao aliye majeruhi.