Friday 7 February 2014

AFRIKA NA SAFARI YA KUELEKEA NCHINI BRAZIL.



Afrika na safari ya kuelekea nchini Brazil.
·    Ni katika kinyang’anyiro cha kuwania kombe  la dunia.
·    Macho na masikio ya wapenzi wa soka duniani kuelekezwa Brazil mwaka huu.

Na. Josephat Kaira.




Kamakawaida wewe shabiki mkubwa wa kisima cha burudani tunaendelea kufahamishana habari kemkem za kiburudani  zinazoendelea katika ulimwengu wa burudani  kama tulivyoanza  awali kukufahamisha  kukamilika kwa baadhi ya viwanja vitakavyotumika katika kipute kijacho cha kombe la dunia kwa mwaka huu wa 2014 nchini Brazil sasa tunakufahamisha vikosi vya timu shiriki na nyota wake na leo hii tunaanzia na wawakilishi toka barani afrika ambapo bara hilo linawakilishwa na timu tano.

Cameroon   simba wasioshindika  simba wanyika  ni miongoni  mwa timu zitakazo iwakilisha Africa katika michuano hiyo huko brazil ikiongozwa na kocha Volker  Finke na itakuwa ikimtegemea zaidi nyota wake Samwel etoo Phil anayekipiga kwenye club ya Chelsea ya England kama chachu ya ushindi pamoja na wachezaji wengine kama akina Steven mbia anayecheza soka la kulipwa kwenye club ya Olympic maseyii ya nchini ufaransa,joel matip anayekipiga na shalke 04 ya ujerumani na wengineo wengi.

Timu ya Taifa ya Cameroon

Ghana maarufu kama black stars brazil ya Africa mashabiki wa soka barani Africa waliweza kuthubutu kuiita hivyo kutokana  na soka ya kutandaza pasi za uhakika itaongozwa na kocha James Kwesi Appiah na watakuwa  na vifaa wao akina Michael essien Asamoa Gyan Sule muntari na wengineo wao watakuwa kundi  G na timu za  ujerumani,ureno pamoja na marekani.

 Timu ya Taifa ya Ghana

Ivory coasty hawa ni tembo maarufu wakifahamika hivyo ni timu nyingine itakayo iwakilisha Africa katika michuano hiyo ya kombe la dunia kwa mwaka 2014 nchini brazil itakuwa ikinolewa na  Sabri lomauchi na ikiwategemea nyota wake kama Didier drogba Yaya toure nduguye kolo toure itakuwa kundi c pamoja na timu za  Colombia,Ugiriki na japani.

Timu ya Taifa ya Ivory Coast

Algeria maarufu kama mabwea wa jangwani  fennec   foxes  hawa ni wawakilishi wengine kutoka kaskazini mwa bara la Africa wakiwa na kocha wao Vahid  Halihodzic na watakuwa wakiwategmea akina  majid boughera anayekipiga kweny club ya  lekhwiya,ryad  boudebouz anayekipiga katika timu ya bastia ya nchini ufaransa ambapo watakuwa na upinzani mkali na timu za  urusi ubelgiji na jamhuri ya watu wa korea katika kundi h.

 Timu ya Taifa Algeria

Nigeria super eagles wakiwa na kocha mzalendo na aliyepata mafaniko makubwa na timu hiyo kwa siku za karibuni baada ya kunyakuwa ubingwa wa Africa Steven keshi wao watakuwa na matumaini makubwa kwani wanajivunia kikosi kilichosheheni nyota kibao wanaosakata kandanda la kulipwa barani ulaya kama akina John mikel Obi,Uche, mlinda mlango Vicent Enyeama na wengineo  ambao watakuwa nchachu ya ushindi katika mechi zao za kundi  f wakiwa na timu za Argentina,Boznia and Herzegovina na iran.

 
Timu ya Taifa ya Nigeria

No comments:

Post a Comment