Tuesday 30 July 2013

HAPA NI WAKATI WACHEZAJI WA STARS WAKIJIANDAA KWENDA UGANDA KUPAMBANA NA THE CRANES MECHI YA CHAN


KICHAPO ILICHOKIPATA STARS KUTOKA KWA WAGANDA, CHAZIDI KUWAPASUA VICHWA WAPENZI NA MASHABIKI WA SOKA NCHINI TANZANIA;

·        Wasema Stars haina jipya, ni sawa na ‘maiti’ ile ile ila sanda tofauti

·        Lawama lukuki zaelekezwa kwa TFF

                         Na. deo kaji makomba.

Kipigo ilichokipata timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa stars, kutoka kwa timu ya soka ya taifa ya Uganga The Cranes, cha mabao 3 – 1, wikiend iliyopita huko kwenye uwanja wa Nambole Kampala nchini Uganda kimezidi kuwapasua vichwa wapenzi na mashabiki wa soka nchini, huku wakisema kuwa  bado kuna safari ndefu katika kandandanda la Tanzania.

Wakizungumza  kwa nyakati tofauti na Kisima cha habari, wapenzi na mashabiki wa soka nchini wamesema kuwa bado kuna kazi kubwa kwa soka la Tanzania kutokana na kiwango ilichokionesha Stars jumamosi iliyopita na hivyo kupelekea kuondolewa katika harakati za kuwania tiketi ya kuelekea nchini Afrika ya kusini katika fainali za  CHAN zinazotarajiwa kufanyika hapo mwakani.

Miongoni mwa wapenzi na mashabiki hao aliyezungumza na Kisima cha habari ni John Mwambigija, ambaye amesema kuwa hakuna jipa katika kikosi cha Stars kutokana na kutokuwepo na program endelevu katika soka la Tanzania.

Mwambigija ambaye pia ni muhadhiri katika chuo cha biashara CBE, Campus ya Mwanza amesema, timu ya soka ya taifa ya Tanzania haina jipya, kutokana na shirikisho la soka nchini Tanzania, TFF, kushindwa kuwa na program ya muda mrefu hali inayoifanya timu hiyo kutokuwa na jipya.

“Unajua ndugu mwandishi, hii ni sawa na maiti ileile ila sanda tofauti, yaani wachezaji walewale ambao hawana jipya ila mashindano tofauti.” Alisema Mwambigija.

Aidha Mwambigija ameongeza kusema kuwa lawama za kushindwa kupaa kwa soka la Tanzania zinapaswa kuliangukia TFF, kutokana na shirikisho hilo kushindwa kuzingatia program ya soka la vijana na hivyo Tanzania kushindwa kuzalisha wachezajiwapya na hivyo kubaki na kizazi kilekile.

“Kikowapi kikosi cha Copacoca cola cha Tanzania kilichotisha Brazil takriban miaka saba iliyopita? Alihoji Mwambigija na kuongeza kuwa TFF haikuwa na mpango wowote wa kuwalea wachezaji hao ambao wangekuwa tegemeo kwa badae katika soka la Tanzania.

Shabiki mwingine kuzungumza na Kisima cha habari ni Christian Ndunguru, ambaye yeye amesema kuwa matokeo mabaya ya stars yanatokana na Tanzania kukosa mizizi ya soka hivi sasa.
Ndunguru amesema kuwa kuwa hakuna ukuzaji na  mwendelezo wa vipaji vya soka la Vijana nchini, kiasi kwamba soka la Tanzania kutoboa  itakuwa ni sawa na ndoto za alinacha.

“Hebu angalia mwandishi mashindano kama ya Copa Coca Cola na haya ya Airtel Raising Stars yana malengo mazuri isipokuwa baada ya hapo, wachezaji wanopatikana hawaendelezwi.” Alisema Ndunguru mkazi wa National jijini Mwanza.

Kila mara mipango ya timu ya soka ya Taifa ya Tanzania, taifa stars, ya kutaka kusonga mbele katika mashindano mbalimbali ya soka imekuwa ikigonga ukutaa, ikiwemo ile safari ya kuelekea nchini Brazil hapo mwakani katika fainali za kombe la dunia, na safari hii ikiondolewa na Uganda katika safari ya kuelekea fainali za CHAN nchini Afrika Kusini hapo mwakani.

Wakati huohuo kocha mkuu wa timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa stars, Kim Poulsen, amesema kuwa amepokea kwa masikitiko makubwa kipigo ilichokipata Stars kutoka kwa Waganda na hivyo kuondolewa katika harakati za kuwania tiketi ya kuelekea katika fainali za CHAN nchini Afrika Kusini, hapo mwakani.
Kocha huyo wa Stars ametoa kauli hiyo jumatatu hii mbele ya wandishi wa habari jijini Dare es salaam,  mara baada ya kuwasili kwa kikosi hicho kutokea mjini kampala nchini Uganda, huku Stars ikiiondoshwa katika safari ya kuelekea fainali za CHAN kwa jumla ya mabao 4 – 1 na The Cranes. 
                                        Kim Poulsen, kocha mkuu wa Stars

 Poulsen amesema kuwa licha ya kupoteza nafasi ya kuelekea katika fainali za CHAN, sasa mipango yake anaielekezea katika fainali za michuano ya fainali 2015.

NALO KANDANDA LA WANAWAKE HUKO BARANI ULAYA !



WANAWAKE WA UJERUMAN WATAWAZWA MABINGWA WA SOKA BARANI ULAYA MWAKA HUU.

Na. deo kaji makomba

Mlinda mlango wa timu ya soka ya taifa ya wanawake ya Ujerumani, Nadine Angerer aliokoa mikwaju muiwili ya penalt na kusaidia taifa lake kuweza kutwaa ubingwa wa Ulaya kwa upande wa wanawake kwa mafanikio mara sita.

Wanawake wa Ujerumani wametwaa uchampion huo kwa kuwavurumsha Norway kwa mikwaju ya penalt katika mechi ya fainali uliopigwa mjini Stockholm Sweden.
 Mlindamlango wa timu ya taifa ya wanawake ya ujerumani, Nadine Angerer, akishangilia ushindi. Nadine aliokoa penalti mbili katika mchezo wa fainali wa Euro kwa wanawake.

BARANI ULAYA NA MANDALIZI YA VILABU KUELEKEA MISIMU MIPYA YA LIGI KUU



SEKESEKE LA USAJILI WA  WACHEZAJI WA SOKA  BARANI ULAYA;
·     Dau la paun milioni 85 “lamdatisha” Bale
·     Ataka Spurs wafanye mazungumzo na Madrid
            
         Na. deo kaji makomba.

Mchezaji wa timu ya soka ya Tottenham Spurs ya Englang, Gareth Bale, ameonesha nia yake ya kutaka kuzungumza na klabu ya soka ya Real Madrid ya nchini Uispania ili kuona uwezekano wa kuichezea klabu hiyo, lakini mwenyekiti wa Spurs Daniel Levy amesema katu mshambuliaji huyo hatouzwa katika Real Madrid.

Madrid tayari walikwishawasilisha mkataba wa kimandishi wakimtaka mshambuliaji huyo,ingawa Spurs imesisitiza kuwa bado mawazo yake ni kuendelea kubaki na na Bale mwenye umri wa miaka 24, licha ya kwamba wamepokea  mkataba mnono uliovunja rekodi ya dunia wa paun million 85.

Tottenham wana matumaini ya kumshawishi Bale kukamilisha mwaka wake mmoja uliosalia katika mkataba wake wa miaka mitatu na timu hiyo ya England.
Bale alijiunga na Spurs akitokea klabu cha soka cha Southampton kwa dau la pauni milioni kumi mnamo mwaka 2007.

Madrid  wanatarajia kuendelea na nia yao katika wiki ijayo na kuwataka Tottenham kumuachia mchezaji huyo ambaye alikwamisha wavuni jumla ya magoli 26 katika mashindano yote msimu uliopita.


 Mshambuliaji wa kimataifa gareth Bale anayeliliwa kwa udi na uvumba na Real Madrid ya Uispania, akiwa katika pozi.

Tottenham ilirejea  mjini London jumapili iliyopita ikitokea katika mandalizi yake ya mwishomwisho ya kindumbwendumbwe cha ligi kuu ya soka ya England huko nchini Hong Kong. Bale hakucheza katika mechi yoyote  katika ziara hiyo barani Asia kutokana na tatizo la msuli.

Mnamo mwezi mei mwaka huu wakala wa Bale, Jonathan Barnett aliiambia televishen ya nchini Uispania mteja wake atafarijika kusikia kutoka kwa rais wa Real Madrid, Florentino Perez.

Kwa Madrid kuendelea na nia yake, kwa upande wa Bale wikiend hii wametoa taarifa muhimu kwa Spurs anahitaji kuwepo na uwezekano wa mazungumzo ya kuondoka kuelekea Uispania.

Ijumaa iliyopita, meneja wa Spurs, Andre Villas- Boas alikataa katakata kujibu maswali kuhusiana na hali iliyopo hivi sasa kuhusiana na mchezaji huyo kutakiwa na Madrid, mbali na kusema kuwa mkataba ndio unaozungumza na wanaendelea na  mshambuliaji huyo ambaye alishinda tuzo ya mchezaji wa kulipwa ya mwaka,  inayotolewa na chama cha soka cha England, FA, pamoja na ile ya mchezaji chipkizi katika msimu uliopita.
                                                             
Bado inaonekana kuwa Bale ataichezea timu yake ya Tottenham katika mchezo wake wa kirafiki dhidi ya Monaco ya Ufaransa wikiendi hii, lakini huko uispania, meneja mpya  wa Madrid Carlo Ancelotti anajiandaa na ujio wa mchezaji huyo ambaye akichukuliwa na Madrid atakuwa amevunja rekodi ya kusajiliwa kwa dau kubwa.

Jumamosi iliyopita, Ancelotti alimtoa Cristiano Ronaldo katika upande wa kushoto na kumpa majukumu ya kucheza katikati wakati wa mchezo wa kirafiki wa kimataifa kujiandaa na ligi ya Uispania wakishinda dhidi Paris St-Germain nchini Sweden huku kocha huyo raia wa Uitaliano akijaribu kutafuta mfumo mpya ambao utawajumuisha wote Bale na Ronaldo.