Sunday 6 October 2013

NI MAJANGA KWA VILABU VYA TOTO NA PAMBA VYA MWANZA.



 Kikosi cha timu ya Toto African ya Mwanza, kilichoshiriki ligi kuu mwaka jana. Timu hiyo iko katika harakati za kutaka kurejea ligi kuu msimu ujao.(Picha na maktaba ya Kisima cha habari)

 Matumaini ya timu za Toto na Pamba kutaka kurejea ligi kuu ya soka ya Vodacom hapo mwakani yafifia


  •   Ni baaada ya kufanya vibaya katika mechi za ligi soka daraja la kwanza

  •  Wadau wa soka Mwanza wakitupia lawama chama cha soka mkoani Mwanza, MZFA                  

                                     
                                  Na. Mashaka Baltazar, Mwanza.


UNAWEZA Kusema kwa lugha rahisi na nyepesi kuwa haya ni majanga,baada ya kufifia kwa matumaini ya timu za Toto African na Pamba za Jiji la Mwanza, kufuzu kucheza Ligi Kuu ya soka ya Vodacom katika msimu ujao hapo  mwakani.





Matumani ya timu hizo yamezidi kufifia baada ya kushindwa kufanya vizuri katika michezo yake mwishoni mwa wiki iliyopita baada ya Toto waliokuwa nyumbani kwenye uwanja wa CCM Kirumba,kulazimishwa sare ya mabao 2-2 dhidi ya vinara wa ligi hiyo,Kanembwa JKT ya Kigoma.





Wakati hali ikiwa hivyo kwa Toto, Pamba nayo iliangukia pua baada ya kuchapwa  katika mechi iliyofanyika kwenye uwanja wa Ali Hassan Mwinyi, mjini Tabora.





Kabla ya mechi hiyo Pamba ilikuwa imekubali kichapo cha mabao 2-0, kutoka kwa timu ngeni ya Stendi United ya Shinyanga kwenye uwanja wa CCM Kirumba,hali inayotoa mweleko kuwa timu hizo za Mwanza hazina nafasi tena ya kufuzu kwenye ligi hiyo.





Baadhi ya wadau wanaulaumu uongozi wa soka mkoani hapa kutokuwa na mikakati kama iliyopo kwa vyama vingine ya soka, hivyo ni ndoto za alinacha kuweza kuvusha timu kwenda Ligi Kuu hapo mwakani.





Walisema Chama cha Soka Mkoa wa Mwanza (MZFA), kimekosa dira na mipango ya soka na kuhoji mikoa kama Shinyanga ama Kigoma inawezaje kufanya vizuri halafu Mwanza ishindwe ?





Walidai kuwa pamoja na Pamba kuonekana inaungwa mkono na Serikali ya mkoa kuliko Toto, ni wazi haina watu wa mipango na fitna ya soka. Lakini laiti Toto ineungwa mkono kama ilivyo Pamba ni dhahiri ingeweza kuonesha maajabu.





Hadi sasa Toto ina pointi nne baada ya kucheza mechi nne na kupoteza miwili kushinda mmoja na kutoka sare mchezo mmoja. Kadhalika Pamba imeshinda mechi moja, kutoka sare moja na kupoteza mmoja.





Viongozi wa MZFA hawakupatikana kuzungumzia mstakabali wa timu hizo za Mwanza, baada ya simu ya Mwenyekiti Jackson Songora kutokuwa hewani kila  ilipopigwa na mwandishi wa habari hizi.





MASKINI TOTO AFRICAN JENGO LAKE KUPIGWA MNADA!

Jengo la klabu ya Toto African ambalo linatakiwa lipigwe mnda ili kufidia deni la mkopo wa sh.13 milioni.Jengo hili liko katika mitaa ya Bantu na Kishamapanda.(Picha na Mashaka Baltazar)

Jengo la timu ya Toto African ya Mwanza kuuzwa.

  •     Kulipa deni la hilingi milioni 13 wanazodaiwa.

  •     Uongozi wa timu hiyo wasema, ni njama za kutaka kuliuza.

                        
                          Na. mashaka baltazar, Mwanza.
WAKATI timu ya Toto African,ikikabiliwa na ukata wa fedha na kutokuwa na uongozi wa kudumu, kuna habari za kutaka kuuzwa kwa jengo la klabu hiyo.

Toto inamiliki jengo moja lililopo katika makutano ya mitaa ya Bantu na Kishamapanda, katikati ya Jiji la Mwanza,ambalo sasa linataka kuuzwa ili kulipa mkopo wa sh. 13 milioni .

Fedha hizo zilikopwa na uongozi wa klabu hiyo, kwa ahadi ya kuzirejesha mara baada ya kumalizika kwa Ligi Kuu msimu uliopita,baada ya kulipwa fedha zao na wadhamini wa ligi hiyo kampuni ya Vodacom .

Akizungumza na Kisima cha habari, msemaji wa klabu hiyo Omar Mbalamwezi,aliseam anasikitishwa kuona wajanja wachache wanataka kuuza mali ya jamii.

Alidai haiwezekani jengo hilo ambalo thamani yake ni zaidi ya sh. 200 milioni likauzwa ili kufidia mkopo wa milioni 13,ukizingatia  wajanja wameongeza kiasi kingine cha sh.3 milioni bila sababu na huu ni wizi wa mchana.

“Baadhi ya watu wamekuwa madalali wanataka kuuza jengo la klabu kwa sh.13 milioni ambazo tulikopeshwa na mdau mmoja bila riba,leo wao wameback date na kuongeza deni sasa limefikia sh. 18 milioni na tayari wamepata wanunuzi kwa bei y ash 200 milioni,”alisma Mbalamwezi

Alieleza kuwa anachofahamu kabla ya hatua hiyo,walikutana na mdai wakakubaliana akate fedha hizo kutoka kwa wapangaji wa jengo hilo hadi deni lake la sh.13 milioni liishe,  lakini anashangazwa kuona makubaliano yanakuwa kinyume.

“Kwa mfumo tulio nao Katibu wa klabu ni mwajiriwa na jengo ni mali ya jamii hata kama ni la klabu, bado ni ya jamii, hivyo haliwezi kuuzwa kwa deni la sh.13 milioni,”alisema

Msemaji huyo alidai kuwa kutofanyika kwa mambo mbalimbali na uongozi kumaliza muda wake, kunaifanya timu hiyo iikose misaada kutoka kwa watu wenye mapenzi na maendeleo ya mpira.

“Uongozi umemaliza muda wake,wanachama hawana taarifa ya mapato na matumizi,hakuna mkutano uliyoitishwa kuwaeleza kilichosababisha tmu kusahuka na taarifa ya msimu mzima.Yote hayo hayajafanyika na watu wanaotaka maendeleo ya soka hawapendi hivyo,”alisema Mbalamwezi

Alidai kutokana na klabu hiyo kutokuwa na uongozi wa kudumu baada ya kushindwa kufanya uchaguzi kwa kutumia katiba ya zamani, wamekubaliana waikabidhi timu kwa Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana, ateuwe uongozi wa muda.

Alisema wameshindwa kukabidhi mzigo wa vifaa hivyo vyenye thamani ya sh. 50 milioni kwa kukosa uongozi wa kusimamia rasilimali hiyo ambayo itainufaisha klabu yao.

Mbalamwezi alisema uongozi wa muda utakaoteuliwa,  utasimamia rasilimali za klabu hiyo pamoja na mradi wa kuuza vifaa vya michezo,kutokana na kusaini mkataba wa miaka 10 wa uwakala wa kampuni ya Insegere Sports ya Marekani .

“Rasilimali tayari zipo,lakini unamkabidhi nani asimamie kuuza mzigo huo wakati huna uongozi.Tumeshindwa kuchagua viongozi sababu watu wanadai katiba mpya.Hivyo bora tukabidhi timu kwa DC tukisubiri uchaguzi,”alisema Mbalamwezi