Tuesday 13 August 2013

UUNGWANA NI VITENDO.

Ibrahim Boubacar keita
 Ibrahim Boubacar Keita, rais wa Mali aliyeshinda katika duru ya pili ya uchaguzi nchini humo.

Uchaguzi wa urais wa duru ya pili nchini Mali.

  • Soumalia Cisse aonesha uungwana, akubali matokeo
  • Asema bwana Keita alishinda uchaguzi huo kihalali
  • Amfuata bwana Keita nyumbani kwake kumpongeza



            Na. deo kaji makomba,  

                    na mashirika ya habari.



Mgombea urais nchini Mali, Soumalia Cisse ameonesha uungwana kwa  kukubali kushindwa na mpinzani wake Ibrahim Boubacar Keita katika duru ya pili ya uchaguzi  uliofanyika Jumapili, nchini humo.

Akizungumza Jumatatu  jioni Cisse alisema bwana Keita alishinda uchaguzi huo kwa njia halali na kumtakia kila la kheri.

Msemaji wa bwana Keita, Mamadou Camara ,alisema matokeo yanaonyesha kuwa, alipata kati ya asili mia 70 na 80 ya kura.


Camara alisema bwana Cisse alimtembelea Keita nyumbani kwake Jumatatu jioni na kumpongeza kufuatia ushindi huo.

Aidha, Jumanne hii, msemaji huyo  alisema kuwa ushindi wa bwana Keita ulikuwa mkubwa na kwamba sasa ataelekeza nguvu zake zote katika kuleta maridhiano ya kitaifa nchini Mali.

No comments:

Post a Comment