Tuesday 13 August 2013

KUELEKEA MSHIKEMSHIKE WA LIGI KUU YA SOKA YA ENGLAND.




Marouane chamakh “aikacha” Arsenal na kukimbilia Crystal Palace

Na. deo kaji makomba

Huko nchini England klabu cha kandanda cha Crystal Palace kimefanikiwa kumsajili mshambuliaji wa kimataifa wa Morocco, Marouane Chamakh kwa mkataba wa kuichezea timu hiyo kwa kipindi cha mwaka mmoja.

Mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Morocco mwenye umri wa miaka 29, atakuwa akivaa jezi namba 29 mgongoni, baada ya kukamilisha mchakato wa kuchukua vipimo vya kitabibu.

Awali Chamakh alisaini mkataba na washika bunduki hao wa London, Asernal the Gunner mnamo mwaka 2010, akijiunga na klabu hiyo kwa uhamisho wa bila malipo kutoka klabu cha kandanda cha Bordeaux, lakini baada ya kufunga magoli 11 wakati akiwa katika mwaka wake wa kwanza huko London.

Shamakh alitolewa kwa mkopo kwenda West Ham hapo mwezi januari mwaka huu, lakini alicheza mechi tatu.
Mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Morocco, ni mshambuliaji wa tatu ambaye amesajiliwa katika msimu huu wa kiangazi, akiungana na Kevin Philips aliyesajiliwa bila malipo pamoja na Dwight Gayle kutokea Peterborough

Vijana hao wa Ian Holloway’s wataanza kampeni zao za kuwania ubingwa wa ligi kuu ya soka ya England jumapili hii.

No comments:

Post a Comment