Tuesday 13 August 2013

HAKUSHIKIKI HUKO MISRI


Wandamanaji wanaomuunga mkono rais aliyeondolewa madarakani huko nchini Misri Bwana Mohamed Morsi, wakirushiana mawe na wale wanaounga mkono kuondolewa madaraki kwa kiongozi huyo.


Ni mshikemshike huko nchini Misri.


  •  Polisi watumia mabomu ya machozi kuwatawanya wafuasi wa morsi
  • Chupa na mawe vatumika kushambuliana  kati ya wafuasi wa morsi na wapinzani wake.


                Na. deo kaji makomba

                     na mashirika ya habari


Polisi nchini Misri, wametumia gesi ya kutoa machozi kuwatawanya waandamanaji wanaomuunga mkono rais aliyeondolewa madarakani, Mohammed Morsi wakati wa maandamano yao mjini Cairo.
Vikosi vya usalama viliingilia kati maandamano hayo baada ya wafuasi wa Morsi   kukabiliana na wapinzani  wao wa kisiasa.
Bwana Morsi, aliondolewa madarakani na viongozi wa jeshi mwezi Julai mwaka huu, kufuatia maandamano makubwa.

Walioshuhudia vurugu hizo wamesema kuwa wafuasi wa bwana Morsi na wale  wanaounga mkono serikali ya mpito walirushiana mawe na chupa huku watoto na wanawake wakikimbia kuokoa maisha yao.
Kutokana na ghasia hizo, jeshi nchini Misri limeweka serikali ya mpito.
Wafuasi wa Morsi aliyeingia madarakani baada ya vuguvugu la kiisilamu la Brotherhood kushinda uchaguzi wa rais, wanakataa kukubali serikali mpya ya mpito wakisisitiza kuwa lazima rais wao arejeshwe madarakani.


Vurugu za Jumanne hii zilianza wakati wafuasi wa Morsi, walipotembea hadi sehemu moja ya Cairo ambako watu wengi wanapinga vuguvugu la Muslim Brotherhood.
Waandamanaji hao walijaribu kuingia katika ofisi za wizara moja ingawa polisi waliwalazimisha kuondoka kwa nguvu.
Wakaazi wa eneo hilo walianza kuwakejeli waandamanaji na hapo ndipo polisi walipoingilia mzozo huo.

Mamilioni ya wamisri waliandamana kumtaka Morsi aondolewe mamlakani ingawa wachunguzi wa masuala ya kisiasa wanasema kuwa kuondolewa kwake kunaonekana kuzorotesha migawanyiko ya kisiasa iliyoko kwa sasa.


Wafuasi wake wamekuwa wakipiga kambi mjini Cairo wakitaka arejeshwe mamlakani, ilihali kiongozi wao akiwa kizuizini huku nchi hiyo ikiwa katika serikali ya mpito.

Maafisa wa usalama walitishia kuondoa mahema waliyoweka wafuasi wa Morsi ambako wamekuwa wakipiga kambi lakini wakabatili uamuzi wao baada ya kuamua kuuakhirisha.


No comments:

Post a Comment