Tuesday 13 August 2013

“HATUNA IMANI NA UCHUNGUZI WA PONDA”








Tukio la kupigwa risasi kwa shekh Mponda

·        Watetezi wa haki za binadamu na taasisi mbalimbali za dini, walaani tukio hilo.


·        Wasema hawana imani na uchunguzi kuhusu Mponda


 


        Na. Mwandishi wetu 

                 Dare es salaam.



 

Tukio la kujeruhiwa kwa Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Sheikh Ponda Issa Ponda na kitu kinachodhaniwa kuwa ni risasi mkoani Morogoro kimeamsha hisia tofauti miongoni mwa watetezi wa haki za binadamu na taasisi mbalimbali za dini nchini Tanzania na kuongeza kuwa hawana imani na uchunguzi kuhusu shekh Mponda.

Watetezi wa haki za binadamu nchini Tanzania kupitia kituo cha sheria na haki za binadamu Tanzania pamoja na kulaani tukio la kujeruhiwa kiongozi huyo wa taasisi ya kiisalam wametaka tume ya haki za binadamu na utawala bora nchini kufuatilia pia matukio mengine ambayo inadaiwa  vyombo vya dola vinatumika kuua na kujeruhi raia.

Wakati jeshi la Polisi nchini likitangaza kuundwa kwa timu ya maafisa polisi kupitia timu inayojulikana kama haki jinai, watetezi wa haki za binadamu wamepinga hatua hiyo kwa madai kwamba polisi hawawezi kujichunguza wenyewe.

Nalo Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA)  kwa upande wake limelaani kitendo cha kujeruhiwa kiongozi huyo  wa kikundi cha kiislamu ambaye anadaiwa kutafutwa kutokana na tuhuma za uchochezi baada ya kupewa kifungo cha nje na mahakama moja huko jijini Dar es salaam.

Sheikh Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Alhad Mussa Salum amewaambia waandishi wa habari jijini Dar es salaam kwamba iwapo Polisi mkoani Morogoro wamehusika na kujeruhiwa kwa Sheikh Ponda, basi wamefanya kitendo kibaya ambacho kinaondoa imani ya wananchi kwa jeshi hilo.

Akizungumzia  uhusiano wa Baraza Kuu la Waislamu Tanzania na Taasisi inayoongozwa na Sheikh Ponda, ambayo inadaiwa kutotambuliwa,  Alhad Mussa amesema Bakwata  haina uadui na Sheikh Ponda kiasi cha kumtaka adhurike.
Shekh Mponda Issa Mponda pichani akionekana katika jukwaa akitoa muhadhara

Naye kamanda wa kanda maalum ya kipolisi Dar es salaam Suleiman Kova alithibitisha kujeruhiwa na kulazwa kwa shekhe Ponda katika taasisi ya mifupa MOI jijini Dar es alaam huku akitaka masuala mengine yanayohusiana na kukamatwa kwake kuachiwa kamanda wa polisi mkoani Morogoro.

Akiwa mkoani Morogoro juzi Sheikh Ponda Issa Ponda alijeruhiwa begani na kitu kinachodhaniwa ni risasi wakati Polisi mkoani humo walipokuwa kwenye harakati za kumkamata.


.Awali siku ya Jumapili Mwenyekiti wa Shura ya Maimamu Tanzania, Alhajj Mussa Kundecha, aliwaambia waandishi wa habari mjini Dar es Salaam kuwa endapo serikali haitachukua hatua itakayowaridhisha Waislamu, wataamua kufikiria upya mustakabali wao na serikali ya nchi hiyo.

Sheikh Ponda amelazwa katika hospitali ya Taifa, Muhimbili, mjini Dar es Salaam akiuguza jeraha la risasi huku akiwa chini ya ulinzi wa askari kanzu.

Taarifa za jumuiya hiyo ambayo inajulikana zaidi Tanzania kama Shura ya Maimamu zinasema kuwa Sheikh Ponda ambaye polisi wanasema walikuwa wakimtafuta kwa tuhuma za kutoa matamko ya uchochezi, alisafirishwa usiku kutoka mji wa Morogoro hadi Dar es Salaam zaidi ya kilomita 200.

No comments:

Post a Comment