Monday 12 August 2013

KOMBE LA HISANI HUKO ENGLAND




Manchester United bingwa

·         Yaitandika Wigan Athletics


·         Van Persie azidi safisha nyota kwa Moyes, atupia mbili wavuni.



                Na. deo kaji makomba

Huko nchini England mchezaji Robin van Persie, amemuhakikishia bosi mpya wa mashetani wekundu, timu ya Manchester United, David Moyes kuendelea kuwepo na klabu hiyo, baada ya kuanza msimu huu na kikombe cha ngao ya hisani, kufuatia kipigo ilichokitoa kwa timu ya Wigan athletics kwenye uwanja wa Wembley.

Bosi huyo mpya wa Mashtani wekundu hao wa England, Moyes ametumia muda wake katika msimu huu wa kiangazi kujadili majaliwa ya mshambuliaji wayne Rooney, lakini dimbani katika miaka uliopita Van Perie aliyekuwa aliyekuwa mfungaji bora, kwa mara nyingine ameonesha tofauti.

Ilimchukuwa takribani dakika sita, Van Persie kufungua ukurasa wake katika msimu mpya, akiunganisha kwa kichwa kona fupi  iliyochongwa na Patrie Evra.
 Mhambuliaji wa timu ya Manchester United, akifanya yake jumapili iliyopita katika uwanja waWembley, wakati timu yake ilipoibuka na ushindi katika mchezo wa ngao ya hisani.
 
Wakati Van Persie anaongeza goli la pili kwa Manchester United, ingawa ilikuwa imeshinda inamfanya Moyes kufikiria zaidi kibarua chake kipya vile atakavyoendelea nacho akianza na matokeo mazuri

No comments:

Post a Comment