Sunday 29 December 2013

MOURINHO AITABILIA LIVERPOOL UBINGWA WA LIGI KUU YA ENGLAND.>>>>>>>>>>>

Kocha wa timu ya soka ya Chelsea Jose Mourinho.


Mourinho aitabiria Liverpool kutwaa ubingwa wa ligi kuu ya England.

Na. Deo Kaji Makomba.

Kocha mkuu wa Chelsea Jose Mourinho anaamini kuwa klabu ya Liverpool ndiye bingwa wa ligi kuu ya England kwa msimu huu kwani kwa sasa Kocha wa timu hiyo Brendan Rodgers atakuwa na kazi moja ambayo ni kuangazia ligi hiyo.

Mourinho anahisi Liverpool kutoshiriki mashindano ya Klabu Bingwa Ulaya itawasaidia kunyakua kombe hilo walilolikosa kwa miaka 24 iliyopita.

"Hawashiriki kwenye joto la mashindano ya Klabu Bingwa Ulaya wala ya Europa league Mourinho," amesema.

"Ubora wa timu pamoja na ari hiyo ndio faida yao ni kweli wanaweza kushinda kombe".
Timu za Chelsea, Manchester United, Manchester City na Arsenal wanashiriki mashindano ya Klabu Bingwa barani Ulaya ambapo Mourinho anaamini kwamba Liverpool watamalizia mechi chache kama 20 tofauti na washindani wao kwa msimu huu.

"Hawa wachezaji watacheza mechi zipatazo 60. Liverpool itacheza mechi 40. Hii ni tofauti kubwa sana," aliendelea.

"Liverpool watakuwa kwenye mapumziko kwa msimu mmoja, wiki moja ya kujiandaa kwa mechi, watacheza mechi, wiki moja watajiandaa kwa mechi inayofuata. Hii ina faida, ni manufaa yasiyodhaniwa."

No comments:

Post a Comment