Thursday 26 December 2013

KINDUMBWENDUMBWE CHA LIGI KUU SOKA YA ENGLAND HII LEO.>>>>>>>>>>



Ligi kuu ya soka ya England.
·    Liverpool Uso kwa uso na Manchester City.
·    Ni katika mtihani wa kuwania ubingwa wa ligi kuu hiyo.
·    Viwanja vingine navyo kutimka vumbi Boxing day hii.

Na. Deo Kaji Makomba.

Huko barani ulaya klabu ya soka ya Liverpool ya England huenda ikasalia kileleni mwa ligi kuu ya soka ya England katika sikukuu hii ya Krismas, lakini inakabiliwa na mtihani mgumu ili kujihakikishia kuendelea  kukalia kigoda cha ligi hiyo yenye mashabiki lukuki katika ukanda wa Afrika Mashariki, watakapokuwa wageni katika Boxing day,  mbele ya Manchester City.

 Wakiwa katika nafasi ya tatu kwenye msimamo wa ligi kuu ya kandanda ya England, kwa kuwa na pointi 35 kibindoni,  Manchester City wana asilimia kubwa ya kufanya vizuri katika uwanja wake wa nyumbani wa Etihad, kulingana na rekodi inavyoonesha hadi hivi sasa katika msimu huu wa ligi kuu hiyo.

Arsenal inayoshikilia nafasi ya pili katika msimamo wa ligi kuu hiyo itakuwa ugenini leo alhamis boxing day kupambana na West Ham, wakati Chelsea inayoshikilia nafasi ya Nne watakuwa wenyeji wa Swansea.

Everton walio katika nafasi ya tano watapambana na Sunderland nao Mashetani wekundu timu ya Manchester United wako ugenini kupambana na Hull.

No comments:

Post a Comment