Monday 28 October 2013

ROCK CITY MARATHON YAFANYIKA JIJINI MWANZA




Msanii wa kikundi cha Utamaduni cha Cecilia cha Bujora, akicheza na nyoka aina ya chatu. Alikutwa jana kweny uwanja wa CCM Kirumba wakati wa mbio za Rocky City Marathon.
Klabu ya riadha kutoka mjini Moshi mkoani Kilimanjaro yatamba Rock city Marathon.

                           Na. Mashaka Baltazar.

WAFUKUZA upepo wa Klabu ya Riadha ya Holili Youth Athletics ya Moshi (HYAC), wameitoa kimasomaso Tanzania, katika mashindano ya mbio ndefu za Rocky City Marathon.

Katika mashindano hayo ambayo yalifanyika jijini Mwanza jumapili iliyopita, wanariadha wa klabu hiyo walishika nafasi ya kwanza, ya pili kwa mbio za Kilomita 21 wanaume na kuwashinda wapinzani wao wakiwemo raia wa Kenya,ambapo Sara Ramadhani alishika nafasi ya pili kwa wanawake.

Akizungumza na Kisima cha habari kuhusiana na ushindi huo, Mkurugenzi wa Holili Youth,Domician Rwezaura, alisema mafanikio hayo yametokana na juhudi na mazoezi ya wanariadha wa klabu hiyo pamoja na kujituma.

Alisema baada ya kutofanya vizuri mwaka jana walijipanga na kufanya mazoezi  wakilenga kulinda vipaji vyao lakini pia kujiandaa na mashindano mbalimbali.

“Ni ushindi wa kujivunia ukizingatia Rock City Marathon ni mashindano ya Kimataifa,yanayoshirikisha wakiambiaji kutoka nje ya  nchi. Ingekuwa aibu kwa Tanzania zawadi zote za kwanza kunyakuliwa na wageni,”alisema Rwezaura

Alitoa rai kwa waandaaji wahamasishe mchezo wa riadha nchini badala ya kuangalia mapato, kiwezkana wadhamini nao kwa upande mwingine wajitokeze kuhammasiha jamii kuupenda na kuthamini mchezo huo.

Mwanariadha Alphoncce Alex wa Holili,alishika nafasi ya kwanza mbele ya Mkenya Joel Kimtae ,akitumia muda wa saa 1:02:17 na kuuvunja rekodi ya mwaka jana ya saa 1:04 iliyowekwa na Dickson Marwa.

Nafasi ya tatu mbio hizo za Kilomita 21 ilinyakuliwa na Sambu Andrew wa Holili.Upande wa wanawake nafasi ya pili ilitwaliwa na Sara Ramadhan wa Holili, nyuma ya Victoria Chepkemoi wa Kenya,ambapo Zakia Mrisho alishika nafasi ya tatu na wanne alikuwa na Damaris Aleba.

Wambura Lameck wa Holili alishika nafasi ya kwanza kwa wanaume,wa pilii Dottto Ikangaa na wa tatu alikuwa ni Juma Nyang’au, mbio za Km 5, huku Neema Mathias pia wa Holili akishika nafasi ya pili.

Mshindi  wa kwanza wanaume mbio za km 21,alizawadiwa sh.1.5 milioni na tiketi ya ndege, wa pili sh.900,000 na king’amuzi na watatu alipata sh.700,00 na king’amuzi.

Kwa upande wa wanawake zawadi zilikuwa sh.1.5, wa pili sh.900,000 na king’amuzi,wa tatu sh.00,000 na kingamuzi,ambapo washiriki wengine walioshika nafasi ya nne hadi ya kumi walipata kifuta jasho.

Wadhamini wa mashindano hayo Kampuni ya mawasiliano ya Airel na mfuko wa hifadhi ya Jamii, (NSSF) kwa nyakati tofauti walisema mashindano ya mwaka huu yamekuwa na hamasa kubwa kutokana na washiriki wengi kujiokeza.

“Mashindano haya yako katika ngazi ya Kimataifa na yamekuwa na hamasa kubwa mwaka huu,yamevuta washabiki wengi ambapo yameshirikisha  watoto, wazee na watu wenye ulemavu,”alisema Jackson Mbando..

“NSSF tumekuwa wadhamini wa Rock City Marathon tangu miaka mitano Iliyopita, pamoja na kuwa na  mafao ya ulemavu kazini ,lakini tumelenga kuhamasisha jamii kuona umuhimu wa kushiriki riadha na kuibua vipaji,”alisema Eunice Chiume,Meneja Mawasiliano Kiongozi wa NSSF

Mashindano ya mwaka huu ambayo yalikuwa ya umbali wa km 2.5,km 5 na km 21 yalishirikisha watoto wa umri wa miaka 7 hadi 10,wazee,walemavu wafanyakazi wa taasisi mbalimbali na wanariadha wnye umrii tofauti tofauti.


No comments:

Post a Comment