Wednesday 14 August 2013

BADO NI HATARI HUKO NCHINI MISRI

Afisa wa usalama wa Misri anazungumza na mwanamke anaeshikilia mti katika kambi iliyoshmabuliwa na vikosi vya usalama. karibu na chuo kikuu cha Cairo huko Giza, Cairo, Misri, Jumatano
Afisa wa usalama wa Misri anazungumza na mwanamke anaeshikilia mti katika kambi iliyoshmabuliwa na vikosi vya usalama. karibu na chuo kikuu cha Cairo huko Giza, Cairo, Misri, Jumatano


Misri yatangaza amri ya dharura

  •  Yaelezwa watu 2,200 wameuwawa
  •  Jeshi laamrishwa kusaidia kutanzua mzozo
 

                    Na. deo kaji makomba,
                         na mashirika ya habari


Serikali ya Misri imetangaza amri ya dharura nchini kote kuanzia hii leo jumatano, kwa muda wa mwezi moja kufuatana na taarifa ya rais iliyotangaza na televisheni ya taifa.

Taarifa hiyo ina liamrisha pia jeshi kukisaidia kikosi cha polisi ili kuweza kutanzua mzozo huo unaotapakaa kote Misri.

Taarifa hiyo imetolewa wakati vikosi vya usalama vilikuwa vinashambulia makambi mawili kuwaondowa wafuasi wa rais aliyeondolewa madarakani bwana Mohamed Morsi katikati ya mji mkuu wa Cairo.

Wakati huo huo kumekuwepo na ripoti zinazotofautiana hii leo juu ya idadi ya watu walouliwa na walojeruhiwa katika ghasia zinazotokea kote nchini.

 Wizara ya afya inaeleza watu 95 wameuliwa na wengine 974 kujeruhiwa kote nchini.

hata hivyo baadhi ya wanachama wa chama cha Muslim Brotherhood cha Bw Morsi wanasema idadi ya walofariki imefikia hadi 2,200 na wengine elfu 10 kujeruhiwa.

No comments:

Post a Comment