Sunday 16 June 2013

SAFARI YA KUELEKEA BRAZIL KOMBE LA DUNIA

                                        
NI PATASHIKA NGUO KUCHANIKA  UWANJA WA TAIFA 
·  Stars uso kwa uso na Ivory cost.
  Na. Deo Kaji Makomba.  

Patashika nguo kuchina nyasi kuwaka moto inatarajiwa kuanza  majira ya saa tisa alasiri, kwenye uwanja wa Taifa jijini Dare es salaam.

Patashika hiyo itazihusisha timu za soka za mataifa ya Tanzania na Ivory Cost, ikiwa ni mpambano  katika harakati zile za kuwania kucheza fainali za kombe la dunia hapo mwakani huko nchini Brazil.

Tayari homa ya pambano hilo imekwishakupanda miongoni mwa wachezaji wa timu zote hasa kutokana na umuhimu wa mchezo huo katika hatua hii ya lala salama ya kuwania kuelekea kule Brazil kunako michuano hiyo mikubwa duniani ambayo hufanyika kila baada ya miaka minne na kuandaliwa na nchi ambayo inakuwa imeshinda ,katika kura ya nchi gani inayositahili kuandaa mashindano hayo, kulingana na shirikisho la soka duniani, FIFA.

Timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars inateremka uwanjani hii leo huku ikiwa na nia moja tu ya kutaka kushinda mchezo huo ili kuweza kujijengea mazingira mazuri ya safari kuelekea Brazil na hivyo kuzidi kuwaongezea raha watanzania walio na kiu kubwa ya muda mrefu kuona Tanzania inabisha hodi katika medani ya soka duniani.

Endapo kama Tanzania itashinda mchezo wake huu dhidi ya Ivory Cost, itakuwa imejikusanyia pointi tisa na hivyo kuongeza matumaini ya safari ya Brazil, wakati Ivory cost ikiishinda Tanzania katika mchezo huu itakuwa tayari na pointi kumi na tatu na hivyo kujihakikishia kukwea pipa kuelekea Brazil hapo mwakani.

Kutokana na kila timu kuuchukulia mchezo huu katika umuhimu mkubwa na wa aina yake hapana shaka itakuwa ni mchezo wa patashika nguo kuchanika nyasi kuwaka moto pale, filimbi ya kwanza ikipulizwa kuashiria kuanza kwa mchakato huo wa lala salama wa kuelekea Brazil hapo mwakani kwa nchi za Afrika.

No comments:

Post a Comment