Friday 14 June 2013

HABARI MAHSUSI




Ajali ya Tren na bus yatokea Shinyanga muda mfupi uliopita
 


Habari zilizotufikia hivi punde hapa katika chumba chetu cha habari cha mtandao huu kutoka mjini Shinyanga magharibi mwa Tanzania, zinaarifu ya kuwa kuna ajali mbaya imetokea ikilihusisha basi la abiria Sai Baba lililokuwa likitokea Jijini Dare es salaam kuelekea Jijini Mwanza kugongana na gari moshi la abiria lililokuwa likitokea Jijini Mwanza kuelekea Dare es salaam.
Kulingana na vyanzo vya habari kutoka katika eneo la tukio, vinaeleza ya kuwa ni ajali mbaya imetokea huku majeruhi wakiokolewa na hakuna taarifa yoyote endapo kama kuna watu waliopoteza maisha katika ajali hiyo
Tunafanya juhudi za kumtafuta kwa njia ya simu Kamanda wa Polisi Mkoani Shinyanga Bwana Mangala Evarist ili kupata undani wa taarifa hii. Endelea kufuatila mtandao huu.

No comments:

Post a Comment