Sunday 16 June 2013

SIOGOPI IVORY COST , ASEMA POULSEN.


    Kocha mkuu wa timu ya soka ya taifa ya Tanzania, taifa stars Kim Poulsen akizungumza na wandishi wa habari jiji Dar es salaam.

Na. Deo Kaji makomba.
 
Wakati timu ya soka ya Tanzania,Taifa stars ikishuka uwanjani hii leo kupepetana na Ivory Cost, kocha mkuu wa Stars Kim Poulen, amesema kuwa kamwe haiogopi Ivory Cost na kwamba vijana wake wataingia uwanjani kwa lengo la kupambana  bila kuangalia ama kujali majina na historia ya soka iliyonayo, nchi hiyo.

Kocha Poulsen ametoa kauli hiyo wakati akizungumza katika mkutano  na wandishi wa habari hapo jana Jijini Dare es salaam.

Poulsen amesema kuwa haiogopi Ivory Cost isipokuwa anaiheshimu timu hiyo kutokana na kuwa ni miongoni mwa timu bora za soka barani Afrika  ila ana imani kubwa na kikoisi chake kutokana na wachezaji wake kuendelea kubadilika siku hadi siku na kuonesha viwango vizuri vya uchezaji  hivyo wanaingia uwanjani wakitunisha vifua ili kuwakabili bara bara tembo hao wa Ivory Cost na ikiwezekana kuwachakaza.

Katika mkutano huo pia, Poulsen alitumia kuwatoa wasiwasi watanzania kuhusu mbadala wa mshambuliaji Mrisho Khalfan Ngasa, ambaye hatatinga dimbani katika mechi hii muhimu kwa Tanzania, upon a kwamba hakuna tatizo, ingawa hakutaka kuweka hadharani ni mchezaji gani atakayesimama badala ya Mrisho kwasababu alizoziita za ufundi katika soka.

Mrisho Khalfan Ngasa, hatacheza mchezo huo kutokana na kuwa na kadi mbili za njano.
Wakati huohuo, shirikisho la soka nchini Tanzania, TFF, limewataka watanzania kujitokeza kwa wingi uwanjani kuishangilia Stars ili kuweza kuwapa moyo na nguvu wachezaji.
Kisima cha habari kinaitakia kila la heri Stars. Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki stars katika mchezo huo

No comments:

Post a Comment