Wednesday 6 November 2013

KINA DADA WA TANZANITE WAKIPASHA MISULI MOTO KABLA YA KUELEKEA MSUMBIJI



Kikosi cha timu ya soka ya taifa ya wanawake chini ya umri wa miaka 20, Tanzanite, kikipasha misuli moto, kabla hakijaelekea Maputo, Msumbiji.
TANZANITE YAELEKEA  MAPUTO MSUMBIJI.


                             Na. Mwandishi wetu.

Kikosi cha timu ya Taifa ya wanawake chini ya miaka 20 (Tanzanite) imeagwa jana jumatano (Novemba 6 mwaka huu) saa chache kabla ya kuanza safari ya kwenda Maputo, Msumbiji.

Hafla fupi ya kuikabidhi bendera Tanzanite imefanyika jana jumatano saa 5 asubuhi kwenye ofisi za TFF wakati kikosi hicho  kikiondoka saa  saa 11 jioni kwa ndege ya LAM na kuwasili Maputo saa 3.45 usiku.

Msafara wa Tanzanite ambayo ilishinda mechi ya kwanza mabao 10-0 karibu wiki mbili zilizopita jijini Dar es Salaam utaongozwa na mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya TFF, Kidao Wilfred.

Mechi hiyo ya marudiano itachezwa Novemba 9 mwaka huu Uwanja wa Taifa wa Zimpeto, na timu itarejea nyumbani Novemba 10 mwaka huu saa 8.30 mchana kwa ndege ya LAM.

No comments:

Post a Comment