Friday 4 October 2013

HALI YA HEWA YACHAFUKA HUKO MOMBASA

Salim Adbi pekee ndiye aliyenusurika kifo


Ghasia zaibuka huko pwani ya Kenya.

·         Ni baada ya mauaji ya mauaji ya Shekh Logo huko Mombasa.

·         Vijana wanaodaiwa kuwa ni wafuasi wa dini ya kiislam wateketeza kanisa

                            
                                      Na. deo kaji makomba na,mashirika ya habari.

Taarifa kutoka mjini Mombasa pwani ya Kenya zinasema kuwa vijana wameteketeza kanisa katika ghasia ambazo zimezuka kufutia kuuwa kwa muhuburi wa dini ya kiisilamu.

 Inaarifiwa mtu mmoja ameuawa kutokana na  ghasia hizo.

Sheikh Ibrahim Omar aliuawa kwa kupigwa risasi akiwa na washirika wake wa watatu
Kulingana na taarifa za kipolisi kutoka mjini Mombasa zinaeleza kuwa muhubiri huyo alikuwa akihubiri katika msikiti uliohusishwa na wanamgambo wa kiisilamu wa Al Shabaab. 

Haijulikani aliyetekeleza mauaji hayo ya usiku wa kuamkia ijumaa hii huku kukiendelea kuwa na hali ya wasiwasi miongini mwa waisilamu na maafisa wa usalama mjini humo.

Sheikh Ibrahim Rogo alikuwa muhubiri katika msikiti alipokuwa akihubiri marehemu Sheikh Aboud Rogo ambaye pia aliuawa kwa kupigwa risasi. Aliuawa na watu wengine watatu walipokuwa wanarejea nyumbani Alhamisi usiku baada ya kuhubiri.
 
Sheikh Rogo alishutumiwa kutoa mafunzo yenye itikadi kali yaliyowashawishi vijana kujiunga na makundi ya kigaidi kama Al Shabaab.

Marehemu Aboud Rogo alidaiwa kuwa na uhusiano na kundi la kigaidi la Al Shabaab
Mauaji haya ni sawa na ya marehemu Aboud Rogo Mohammed mwaka jana na ambayo yalisababisha ghasia mjini humo. 


                                                    Marehemu Aboud Rogo

Yanakuja wiki mbili tu baada ya shambulizi la kigaidi lililofanywa dhidi ya jumba la maduka la Westgate ambapo watu 67 waliuawa

Kundi la kigaidi la al-Shabab lilikiri kufanya mashambulizi hayo ya kigaidi.

Aboud Rogo alidaiwa kuwa na uhusiano na kundi la kigaidi la al-Shabab na baadhi ya waisilamu walioshutumu polisi waliomuua walisema kuwa yalikuwa madai tu wala.

Ibrahim Rogo alionekana kama mrithi wa marehemu Aboud Rogo, alipohutubu katika msikiti huo.

No comments:

Post a Comment