Saturday 10 August 2013

MABINGWA WAPYA WA MEYA CUP JIJINI MWANZA HAWA HAPA

Mabingwa wapya wa Meya Cup 2013, timu ya soka ya Isamilo FC, kutoka kata ya Isamilo wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kutawazwa kuwa mabingwa wa mashindano hayo(Picha na Deo Kaji Makomba)


Timu ya kata ya Isamilo yaibuka mabingwa wa Meya Cup

·        Ni baada ya kuibenjua timu ya Mkolani FC kwa mikwaju ya penaiti.



·       Mashindano hayo kuwa ya kudumu

             
       Na. deo kaji makomba

Hatimaye mashindano ya kandanda ya kuwania kombe la Meya jijini Mwanza, maarufu kama Meya Cup, yamefikia tamati  jumamosi hii huku bingwa wa mashindano hayo akipatikana.

Timu ya kata ya Isamilo FC, imeibuka bingwa wa mashindano hayo baada ya kuibenjua timu ya soka ya kata ya mkolani kwa changamoto ya mikwaju ya penaiti 3-1 na hivyo kujinyakulia zawadi ya mshindi wa kwanza.

Katika mchezo huo ulipigwa kwenye uwanja mkongwe wa nyamagana jijini Mwanza ulishuhudiwa timu zote zikitoka uwanjani zikiwa zimefungana bao 1 -1, na hivyo mwamuzi wa mpambano huo, kuamua sheria ya mikwaju ya penaiti ichukue nafasi yake na hatimaye bingwa kupatikana.

Katika fainali hizo zilihudhuria na mamia ya mashabiki wa soka pamoja na viongozi mbalimbvali wakiwemo wa vyama na serikali.

Bingwa wa Meya Cup alizawadiwa Bajaji yenye thamani ya shilingi milioni Nne na pesa tasilimu shilingi 1,500,000, wakati mshindi wa pili akipata milioni tatu, nayo timu ya kata ya Mbugani ikichukuwa nafasi ya tatu na hivyo kujinyakulia zawadi ya shilingi laki tano.

Jumla ya timu 19 zilishiriki katika mashindano hayo, ambapo timu hizo zikitoka katika kata mbalimbali jijini Mwanza pamoja na taasisi mbalimbali ikiwemo timu ya Magazeti FC.

Kwa upande wake msitahiki meya wa halmashauri ya wilaya ya Nyamagana, Stanslaus Mabula, akizungumza na wandishi wa habari mara baada ya kumalizika kwa mechi ya fainali ya mashindano hayo, amesema kuwa mashindano hayo yatakuwa ya kudumu huku lengo lake likiwa ni kuibua na kuendeleza  vipaji vya soka.



No comments:

Post a Comment