Tuesday 6 August 2013

KUELEKEA KIMUHEMUHE CHA LIGI KUU SOKA YA ENGLAND MSIMU HUU



Luis Suarez kuikosa safari ya Liverpool huko Norway kutokana na kuwa majeruhi

 

·        Ni katika mandalizi ya kuelekea kimuhemuhe cha ligi kuu ya soka ya England.

                 

                   Na. deo kaji makomba

Mshambuliaji wa  timu ya soka ya Liver pool ya England, Luis Suarez, ambaye anaonekana kutokutulia,ataikosa ziara ya kimichezo ya kimataifa ya timu yake huko nchini Norway ikiwa ni mandalizi kabla ya kuanza kwa ligi kuu ya soka ya England kutokana na kuwa majeruhi ya mguu.

 Mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Uruguay mwenye umri wa miaka 26, amekuwa akiwaniwa na klabu ya Asernal ambayo tayari imekwishatoa ofa mbili ikitaka kumchukua.

Suarez amekwishacheza mechi tatu katika timu yake ya Liver pool dhidi ya Melbourne victory, Thailand na Olmpiakos.

Kwa upande mwingine pilikapilika za usajili wa wachezaji katika msimu wa majira ya kiangazi huko barani ulaya zinazidi kushika kasi huku wachezaji mbalimbali wakitoka katika klabu moja na kusajiliwa na vilabu vingine, kwa  viwango vikubwa vya fedha.

Miongoni mwa wachezaji ambao tayari wamekwishasajiliwa na vilabu tofautitofauti barani humo, ni Edinson Cavan ambaye anatokea FC Napoli na kusaini Paris St Germain ya Ufaransa kwa dau la paun milioni 55, huku mchezaji Falcao akiachana na Atletico Madrid ya Uispania na kudaka mchongo wa kuichezea Monaco ya Ufaransa kwa dau la pauni milioni 50.

 Mchezaji Ednson Cavan ambaye amesajili PSG ya Ufaransa akitokea FC Napoli ya Italia kwa dau la pauni milioni 55


Wachezaji wengine ni Neymar ambaye anatoka Santos kwenda Barcelona kwa dau la pauni milioni 48.6, James Rodriguez kasajiliwa na Monaco ya Ufaransa kwa dau la pauni milioni 38.5 akitokea Porto ya Ureno, wakati mchezaji Frenandinho akitokea Shaktar Donetsk na kujiunga na Manchester City kwa kitita cha pauni milioni 30


No comments:

Post a Comment