Sunday 23 June 2013

CONFEDARATION CUP


BRAZIL YAIFYATUA ITALIA, MEXCO YAIPIGA JAPANI.

LEO USIKU NI NIGERIA NA UISPANIA, URUGUAY NA TAHIT MECHI ZA KUNDI B


Na. Deo Kaji Makomba

Hekaheka za kuwania kombe la mabara inazidi kuhika kasi huko nchini Brazil, huku timu za mataifa manane zikiendelea kuchuana katika ile hatua ya makundi.

Jumamosi kulishuhudiwa mechi mbili za kundi A zikipigwa huku zikizihusisha timu nne zilizoko katika kundi hilo Brazil, Italia, Mexco na japani.

Matokeo katika kundi hilo hao jana, Brazil iliweza kuibuka na ushindi wa mabao 4-2 dhidi ya Italia wakati Mexco iliishinda Japani 2-1.

Msimamo katika kundi A, mara baada ya mechi mbili za jana jumamosi usiku
                                          

Confederations Cup Group A


P
W
D
L
Pts
GD







Brazil 3 3 0 0 9 +7
Italy 3 2 0 1 6 +0
Mexico 3 1 0 2 3 -2
Japan 3 0 0 3 0 -5


Hekaheka hizo za kuwania kombe la mabara zinaendelea tena usiku wa leo huko nchini Brazil, huku kukishuhudiwa mechi mbili za kundi B zikichezwa.

Wawakilishi wa bara la Afrika, timu ya taifa ya Nigeria inashuka dimbani kupambana usokwauso na timu ya taifa Uispania, wakati Uruguay na Tahit nazo zitakuwa zikioneshana kazi..
 Kikosi cha timu ya soka ya taifa ya Nigeria, kinachoshiriki mashindano ya mabara huko Brazil


Nigeria inaingia uwanjani hii leo kama nyati aliyejeruhiwa, baada ya kukubali kipigo cha mabao2-1 katika mchezo wake uliopita dhidi ya Uruguay, lakini itakuwa ikipambana na miongoni mwa kigogo cha soka duniani, timu ya taifa ya Uispania ambayo inaingia uwanjani huku ikiwa inatakata na ushindi  wa mabao 10-0 dhidi ya timu ya taifa ya Tahit




No comments:

Post a Comment