Thursday 27 June 2013

NI MSHIKEMSHIKE HUKO BRAZIL..



NANI KUUNGANA NA BRAZIL KATIKA FAINALI YA KOMBE LA MABARA?

.Ni Italia au Spain?

Na. Deo Kaji Makomba.

Huko nchini Brazil hekaheka za kuwania kombe la mabara leo hii zinatarajiwa kuendelea tena huku kukihuhudiwa mechi nyingine ya nusu fainali ikipigwa.

Mechi  hiyo kati ya timu ya taifa Spain na Itaria, itapigwa kuanzia majira ya saa mbili usiku kwa saa za Afrika mashariki na ndiyo itakayoamua ni timu ipi itakayoungana na Brazil kucheza fainali hizo.

Timu ya taifa ya Uispania ilifanikiwa kuingia hatua ya nusu fanali ya michuano hiyo baada ya kumaliza hatua ya makundi na kushika nafasi ya kwanza katika kundi B na ikijikusanyia pointi tisa kibindoni wakati Italia ikifanikiwa kuingia katika hatua hiyo baada nayo kumaliza hatua ya makundi kwa kujikusanyia pointi sita.

Tayari wenyeji wa mashindano hayo Brazil, wameweza kufanikiwa kuingia hatua ya fainali baada ya hapo jana usiku (Jumatano) kuichakaza timu ya soka ya taifa ya Uruguay, katika mchezo wa nusu fainali ya kwanza.

Katika mchezo huo Brazil, iliifunga Uruguay mabao 2-1, bao la kwanza likifungwa na mchezaji Fred kunako dakika ya 42 ya mchezo, wakati mlindamlango wa Brazil Cecar awali akiokoa penalty ya Diego Forlan, baada ya David Luiz kumuangusha katika eneo la hatari, nahodha wa timu ya Uruguay, Diego Lugano.
Dakika ya arobaini na nane Uruguay ilinyofoa bao hilo kupitia kwa mchezaji Cavan.

Mpira wa kichwa uliopigwa katika dakika za majeruhi na mshambuliaji wa kimataifa wa Brazil, Paulinho, ndio uliuuwezesha Brazil kuingia hatua ya fainali , katika mchezo huo uliochezwa kwenye  Estadio Mineirao.
Mechi ya fainali ya michuano hiyo inatarajia kupigwa jumapili hii kwenye uwanja wa Maracana, mjini Reo de Janeiro.

Yafuatayo ni majina ya vikosi vya wachezaji waliocheza mechi hiyo ya nusu fainali ya kwanza kati ya Brazil na Uruguay.

Brazil
  • 12 Julio Cesar
  • 02 Alves
  • 03 Thiago Silva
  • 04 David Luiz Booked
  • 06 Marcelo Booked
  • 11 Oscar (Hernanes - 72' )
  • 17 Dias Booked
  • 18 Paulinho
  • 09 Fred
  • 10 Neymar (Dante - 90' )
  • 19 Hulk (Bernard - 64' )
Uruguay
  • 01 Muslera
  • 02 Lugano
  • 03 Godin
  • 16 Pereira
  • 22 Caceres
  • 07 Rodriguez
  • 17 Arevalo
  • 20 Gonzalez Booked (Gargano - 83' )
  • 09 Suarez
  • 10 Forlan
  • 21 Cavani

Wednesday 26 June 2013

KIDUMBWENDUMWE CHA KOMBE LA MABARA HUKO BRAZIL..



NUSU FAINALI YA KWANZA KUPIGWA LEO USIKU, NI BRAZIL NA URUGUAY, SPAIN NA ITARIA ALHAMIS HII.

Na.Deo Kaji makomba.

Harakati za kuwania kombe la mabara almaarufu kama Confedaration Cup, zinazidi kushika kasi huko nchini Brazil, huku timu zitakazocheza hatua ya nusu fainali ya mahindano hayo tayari zikiwa zimejulikana.
Timu hizo ni Brazil, Uruguay, Uispania pamoja na Italia.

Brazil ilifanikiwa kuingia katika hatua hiyo ya nusu fainali baada ya kuongoza kwa kuwa na pointi tisa kibindoni katika msimamo wa kundi A wakati Italia nayo imweza kuingia hatua hiyo ikimaliza hatua ya makundi kwa kuwa na pointi sita.

Nalo kundi B lilimaliza hatua yake ya makundi huku Uispania ikiongoza katika kundi hilo kwa kuwa na pointi tisa na Uruguay ikimaliza hatua hiyo kwa kuwa na pointi sita.

Mechi ya nusu fainali ya kwanza ya mashindano hayo, inazikutanisha Brazil na Uruguay, mechi itakayopigwa kuanzia saa mbili usiku kwa saa za Afrika mashariki.

Nayo nusu fainali ya pili itapigwa alhamis hii, ambapo Uispania itakuwa ikioneshana kazi na Italy.

Ufuatao ni msimamo vile ulivyo baada ya kumalizika kwa mechi hizo za hatua ya makundi ya mashindano hayo ya kombe la mabara ama Confedaration Cup.

Group A
Team
MP
W
D
L
GF
GA
Pts
3
3
0
0
9
2
9
3
2
0
1
8
8
6
3
1
0
2
3
5
3
3
0
0
3
4
9
0


Group B
Team
MP
W
D
L
GF
GA
Pts
3
3
0
0
15
1
9
3
2
0
1
11
3
6
3
1
0
2
7
6
3
3
0
0
3
1
24
0






KUELEKEA LIGI KUU YA SOKA YA ENGLAND.....



PAUNI MILIONI 18 ZAMPLEKA ANDREW SCHURRLE CHELSEA.

·        Sasa kuungana na mjerumani mwenzake, Marko Marin

·        Ni usajili wa kwanza wa Morinho tangu arudi tena Chelsea

     Na. Deo Kaji Makomba

 Barani ulaya klabu ya kandanda ya Chelsea ya Englang, imemsajili mshambuliaji wa kimataifa wa ujerumani Andrew Schurrle, ambaye alikuwa akichezea klabu ya kandanda ya Bayer Liverkusen katika ligi kuu ya soka ujerumani almaarufu Bundedliga kwa dau pauni 18

Schurrle, amekuwa mchezaji wa kwanza kusajiliwa na bosi wa klabu ya Chelsea ya England, Jose Mournho, tangu kocha huyo arejee kwa mara pili katika klabu hiyo iliyoko ligi kuu ya soka ya England, akitokea Real Madrid ya nchini Uispania.

Mshambuliaji huyo wa kimataifa wa ujerumani, amemwaga wino kuichezea Chelsea kwa kipindi cha miaka mitano

“Hii ni heshima kwangu kuichezea klabu hii, na timu hii yenye mashabiki wengi.”Alisema Schurrle.
Mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Ujerumani mwenye umri wa miaka 22, aliweza kuifungia magoli 11 katika mechi 34 za ligi kuu ya soka ya Ujerumani timu yake ya liverkesen kati ya mwaka 2012 na 2013.

Katika michezo hiyo aliyocheza, iliweza kuisaidia klabu yake ya Liverkusen kumaliza ligi ikiwa katika nafasi ya tatu.

Schurrle, ambaye hucheza nafasi ya pembeni au wakati mwingine hucheza kama mshambuliaji wa kati, amefunga mabao saba katika mechi 24 akiwa na timu ya taifa ya Ujerumani na alikuwemo katika cha timu hiyo katika michuano ya Euro 2012.

Scherrle, anaungana na mjerumani mwenzake Marko Marin, ambaye alielekea Stamford Bridge akitokea  Werder Bremen mwezi Julai mwaka 2012, lakini alicheza mechi 12 katika msimu wake wa kwanza.