Friday 7 February 2014

AFRIKA NA SAFARI YA KUELEKEA NCHINI BRAZIL.



Afrika na safari ya kuelekea nchini Brazil.
·    Ni katika kinyang’anyiro cha kuwania kombe  la dunia.
·    Macho na masikio ya wapenzi wa soka duniani kuelekezwa Brazil mwaka huu.

Na. Josephat Kaira.




Kamakawaida wewe shabiki mkubwa wa kisima cha burudani tunaendelea kufahamishana habari kemkem za kiburudani  zinazoendelea katika ulimwengu wa burudani  kama tulivyoanza  awali kukufahamisha  kukamilika kwa baadhi ya viwanja vitakavyotumika katika kipute kijacho cha kombe la dunia kwa mwaka huu wa 2014 nchini Brazil sasa tunakufahamisha vikosi vya timu shiriki na nyota wake na leo hii tunaanzia na wawakilishi toka barani afrika ambapo bara hilo linawakilishwa na timu tano.

Cameroon   simba wasioshindika  simba wanyika  ni miongoni  mwa timu zitakazo iwakilisha Africa katika michuano hiyo huko brazil ikiongozwa na kocha Volker  Finke na itakuwa ikimtegemea zaidi nyota wake Samwel etoo Phil anayekipiga kwenye club ya Chelsea ya England kama chachu ya ushindi pamoja na wachezaji wengine kama akina Steven mbia anayecheza soka la kulipwa kwenye club ya Olympic maseyii ya nchini ufaransa,joel matip anayekipiga na shalke 04 ya ujerumani na wengineo wengi.

Timu ya Taifa ya Cameroon

Ghana maarufu kama black stars brazil ya Africa mashabiki wa soka barani Africa waliweza kuthubutu kuiita hivyo kutokana  na soka ya kutandaza pasi za uhakika itaongozwa na kocha James Kwesi Appiah na watakuwa  na vifaa wao akina Michael essien Asamoa Gyan Sule muntari na wengineo wao watakuwa kundi  G na timu za  ujerumani,ureno pamoja na marekani.

 Timu ya Taifa ya Ghana

Ivory coasty hawa ni tembo maarufu wakifahamika hivyo ni timu nyingine itakayo iwakilisha Africa katika michuano hiyo ya kombe la dunia kwa mwaka 2014 nchini brazil itakuwa ikinolewa na  Sabri lomauchi na ikiwategemea nyota wake kama Didier drogba Yaya toure nduguye kolo toure itakuwa kundi c pamoja na timu za  Colombia,Ugiriki na japani.

Timu ya Taifa ya Ivory Coast

Algeria maarufu kama mabwea wa jangwani  fennec   foxes  hawa ni wawakilishi wengine kutoka kaskazini mwa bara la Africa wakiwa na kocha wao Vahid  Halihodzic na watakuwa wakiwategmea akina  majid boughera anayekipiga kweny club ya  lekhwiya,ryad  boudebouz anayekipiga katika timu ya bastia ya nchini ufaransa ambapo watakuwa na upinzani mkali na timu za  urusi ubelgiji na jamhuri ya watu wa korea katika kundi h.

 Timu ya Taifa Algeria

Nigeria super eagles wakiwa na kocha mzalendo na aliyepata mafaniko makubwa na timu hiyo kwa siku za karibuni baada ya kunyakuwa ubingwa wa Africa Steven keshi wao watakuwa na matumaini makubwa kwani wanajivunia kikosi kilichosheheni nyota kibao wanaosakata kandanda la kulipwa barani ulaya kama akina John mikel Obi,Uche, mlinda mlango Vicent Enyeama na wengineo  ambao watakuwa nchachu ya ushindi katika mechi zao za kundi  f wakiwa na timu za Argentina,Boznia and Herzegovina na iran.

 
Timu ya Taifa ya Nigeria

Thursday 6 February 2014

KUELEKEA KOMBE LA DUNIA NCHINI BRAZIL 2014 MAANDALIZI YA VIWANJA YAENDELEA KUKAMILIKA

Na. Josephat Kaira.


Kama kawaida yetu kisima cha burudani kinaendelea kukupatia mambo mazuri kuhusiana na burudani kitaifa na kimataifa ,zikiwa zimesalia siku chache kabla ya kuanza kivumbi  cha soka cha kombe la dunia kwa mwaka 2014 nchini brazil kitakacho shirikisha timu 32 tumeona ni vizuri tukaanza kukufahamisha viwanja ambavyo vitakuwa vikitumika katika michuano hiyo mikubwa.
Arena de sao  Paulo

Uwanja wa kwanza ni  arena de sao  Paulo,huu ni uwanja ambao uko mjini kabisa katika jiji la sao Paulo hili ni jiji maarufu na lenye idadi kubwa ya watu na linategemewa kubeba idadi kubwa ya mashabiki kutoka kona mbalimbali za dunia  unachukua idadi ya watu  65,807 unamaliziwa vizuri mwezi huu wa februari na cha kukuongezea ni kuwa wakati wa matengnezo yake hivi karibuni uliua wajenzi wawili katika ajali iliyotokea wakati wa ujenzi wa uwanja huo novemba 27 mwaka jana.

Uwanja mwingine utakaotumika katika kipute hicho ha kombe la dunia mwaka 2014 nchini brazil ni estadio mineirao bero herizonte huu ni miongoni mwa viwanjab vikongwe vya soka nchini brazil ulijengwa mwaka 1965 lakini ukafanyiwa ukarabati mkubwa mwaka 2013 lengo likiwa ni kuuweka sawa kabla ya michuano hiyo  kuanza,unachukua mashabiki  62,547 uko miles kutoka rio de geneiro.
 Estadio mineirao bero herizonte

Tukiwa tunendelea kuahamishana viwanja vingine ambavyo vitkuwa vikitumika katika michuano ya kombe la dunia kwa mwaka huu wa 2014 baada ya hivyo viwili vya hapo juu estadio costelao Fortaleza huu ulianza kutumika mwaka 1973 ukafanyiwa ukarabati mkubwa mwaka 2013 unabeba mashabiki wapatao 64,846.
 Estadio costelao Fortaleza

Uwanja  mwingine ni estadio maracana rio de janairo huu ni uwanja mwingine baab kubwa ambao nchi ya brazil itakuwa ikijisifia katika michuano hiyo huko jijini rio de janairo kwa watoto wa mujini vilevile unavikolombezo vingi pia unabeba mashabiki wengi wapatao 76,804 kuzidi ata viwanja vingine tulivyotangulia kukuelezea apo awali.
 Estadio-maracana

Estadio nacional brasilia  huu unachukua mashabiki 68,009 ulifunguliwa mwaka 1974 ila ukaanyiwa tena ukarabati mwaka 2013 mwezi may.
 Estadio-Nacional-de-Brasilia-Julio-Cecilio

Kwa leo tutahitimisha na kukufamisha uwanja wa  arena pernambuco recife huu ni uwanja mpya kabisa ukijengwa hivi karibuni na kufunguliwa mwaka 2013 mwezi may na unachukua mashabiki wapatao 44,248 ni moja kati ya viwanja vitakavyo nogesha michuano hiyo kwani kwa nje kina muwako muwako furani wa kupendeza.


Arena pernambuco recife usiku

Naam kwa wewe unae endelea  kutufuatilia wana kisima cha burudani tutakutajia viwanja vingine vitakavyotumika katika kipute cha kombe la dunia mwaka huu nchini  brazil kadri tuwezavyo endelea kuwa nasi.

Naye mshambuliaji dimitar berbatov amebainisha kuwa mlinzi wa Manchester united mfaransa Patrice evra ndiye aliyemshawishi kujiunga na club ya Monaco katika kipindi cha usajili cha mwezi uliopita wa januari.

  Berbatov

Berbatov raia wa burigaria amesema kuwa rafiki yake evra waliyekuwa wakicheza wote Manchester united kati ya mwaka 2008 hadi 2012 ndiye aliyemwambia mambo mazuri yaliyopo Monaco na kumshawishi kujiunga nayo kwa mkopo akiziba pengo la mkolombia radamel falcao aliye majeruhi.

Saturday 1 February 2014

HARAKATI ZA LIGI YA MABINGWA BARANI ULAYA, MAN CITY KUMKOSA AGUERO>>>>>>>>>>>>>



Sergio   Aguero
Manchester City kumkosa Aguero.
·    Ni katika mechi ya ligi ya mabingwa barani ulaya.
·    Majeraha yamsababisha kukaa nje. Nako nchini Uhispania kocha wa zamani wa soka wa timu ya taifa ya nchi hiyo afariki dunia.

                                              Na. Josephat Kaira.

Kama  kawaida kisima cha burudani kinaendelea kukutaarifu  kuhusiana na  dondoo mbalimbali  za soka kimataifa   ambapo   tukianzia  Uingereza   kunataarifa kutoka  ndani  ya   Klub ya  Mancheter city   ya kuwa   itamkosa  mchezaji wake  Sergio   Aguero   katika  mechi ijayo ya kombe  la mabingwa wa soka barani   ulaya kufuatia  kuwa  majeruhi.

Tayari meneja wa mancheter city  Manuel  Mellegrin    amethibitisha ya  kuwa  Aguero atakaa  nje ya dimba kwa kipindi cha mwezi   mmoja baada  ya  kupata maumivu ya nyonga katika mechi iliyopita dhidi ya tottenham  jumatano iliyopita.

Kutokana na  kuwa majeruhi Aguero  ataikosa mechi  dhidi   ya  Baselona inayotarajiwa kuchezwa februari   18.

Nako nchini Hispania  jumamosi hii   kumeripotiwa  taariafa ya  huzuni  ikimhusu   aliyewahi kuwa kocha wa  timu ya taifa ya nchi hiyo   Luis  Aragones  kufariki dunia mapema asubuhi ya  leo  katika clinic ya  mjini Madrid.
  Luis  Aragones

Taarifa ya kufariki kwa  Aragones   imetolewa  na   dactari   aliyekuwa akimtibu    Pedro   Guiren   ,Aragones ambaye  alikuwa akifahamika kama  Wise man  aliiongoza   Uispania   katika michuaano ya soka  ya ulaya ya mwaka  2008

Aragones   amefariki akiwa na miaka    75   na atataendelea kubaki katika    kumbukumbu ya wapenda  soka  duniani.

Naye bosi wa  timu ya soka ya taifa ya uholanzi Ruiz Van gaal  amethibitiha kuwa amechoka na anafikiria kuustafu kufundisha mchezo wa soka,  mara baada ya kumalizika kwa  michuano ijayo ya kombe la dunia  katikati ya mwaka huu huko  nchini brazil.
 Ruiz Van gaal

Van gaal   ameongeza kuwa miaka miwili aliyokaa kama kocha wa timu ya uholanzi amekuwa kama mgonjwa na amechoka na kibarua hicho  na amefikiria  utakuwa muda muafaka kwake kupumzika mara baada ya kumalizika kwa michuano hiyo ya soka mikubwa duniani.

Nchini  ufaransa kiungo wa  Klub ya  Paris saint german  Blaise  Matuidi  amebainisha   kuwa   yuko kwenye mipango ya kusaini mkataba mpya kuendelea kubaki kwenye Klub hiyo ya nchini ufaransa.
 Blaise  Matuidi

Kiungo Blaise mwenye umri wa miaka 26 amesema ya kuwa anafurahia kuendelea kubakia  Psg  na hakuna ukweli wowote  wa kuwa yuko kwenye mipango ya kutimkia Aserna l ya Uingereza kama ilivyokuwa ikiripotiwa awali.

Naye bosi  Klub ya Fayenoord   Ronard Koeman ameweka  hadharani kuwa ataachana na kibarua cha kuinoa timu hiyo ya uholanzi mwishoni mwa  msimu huu,itakumbukwa ya kuwa koeman amekuwa clubuni hapo kwa muda wa miaka mitatu tangu ajiunge nayo mwaka  2011 akichukua nafasi ya Mario been.
Ronard Koeman
 
Kocha huyo wa fayenoord amesisitiza kuwa anaelewana na kila mmoja kwenye  club hiyo ila ni maamuzi yake binafsi  aliyofikia ya kutosaini mkataba mpya na timu hiyo inayoshiriki ligi kuu ya uholanzi.