Monday 30 December 2013

ERNEST MANGU NDIYE KAMANDA MPYA WA JESHI LA POLISI NCHINI TANZANIA.>>>>>>>

Ernest Mangu, Mkuu mpya wa jeshi la polisi nchini Tanzania. ( Picha na maktaba yetu)


Rais Kikwete amteua Kamishina wa Polisi Ernest Mangu kuwa mkuu mpya wa jeshi hilo.
·    Kuapishwa jumanne hii  viwanja vya Ikulu Dar.
·    Nafasi ya naibu mkuu wa jeshi la polisi yaanzishwa.

Na. Ofisi ya Ikulu.

Rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzanzania Jakaya Mrisho Kikwete leo jumatatu Desemba 30, 2013,  amemteua Kamishina wa Polisi Ernest Mangu kuwa Mkuu wa jeshi la Polisi nchini Tanzania, IGP.

Kulingana na taarifa iliyotolewa na katibu mkuu kiongozi Balozi Ombeni Sefue inaeleza kuwa Kamishina Mangu anachukua nafasi ya mkuu wa Jeshi la Polisi nchini anayestaafu, Said Mwema.

Kabla ya uteuzi wake unaoaanza januari mosi 2014, Kamisha Mangu alikuwa Mkurugenzi wa Intelijensia ya jinai (Director of Criminal Intelligence) katika jeshi hilo la polisi.

Aidha taarifa hiyo inasema kuwa Rais Kikwete amemteua Kamishina Abdulrahman Kaniki kuwa Naibu Mkuu wa wa Jeshi la Polisi nchini Tanzania ikiwa ni nafasi mpya katika muundo wa sasa wa jeshi hilo.

Kabla ya uteuzi wake, Kamishina Kaniki alikuwa Kamishina wa Uchunguzi wa Kijinai (Commissioner  for  forensic Investgations.)

Mkuu wa Jeshi la Polisi mpya ataapishwa jumanne hii Desemba 31, 2013 katika viwanja vya Ikulu jijini Dar es salaam.

Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano,
Ikulu.
Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment