Tuesday 3 December 2013

ASHA ROSE MIGIRO ATEULIWA NA RAIS KUWA MBUNGE.

Aliyewahi kuwa katibu mkuu msaidizi wa Umoja wa mataifa, UN, Asha Rose Migiro, ambaye hivi sasa ameteuliwa kuwa mbunge kupitia CCM.

Nafasi za kuteuliwa za ubunge.
·    Rais amteua Asha Rose Migiro.
·    Uteuzi  huo umeanza tangu jumatatu Desemba 2, 2013.

TAARIFA KUTOKA IKULU.

Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete, amemteua Dr. Asha Rose Migiro kuwa Mbunge.

Taarifa iliyotolewa na Ikulu jijini Dar es salaamjumanne hii ya Desemba  3, 2013, na katibu mkuu kiongozi, Dr. Florens Turuka imeeleza kuwa uteuzi huo umeanza tangu jumatatu ya Desemba 2, 2013.

Dr. Asha Rose Migiro, ni katibu wa halmashauri kuu ya taifa, idara ya siasa na uhusiano wa kimataifa katika chama cha Mapinduzi, CCM.

No comments:

Post a Comment