Friday 18 October 2013

NI PATASHIKA NGUO KUCHANIKA NYASI KUWAKA MOTO WEEKEND HII



 Mashabiki wa timu ya soka ya Yanga wakiwa katika hemwahemwa.

Harakati za kuwania ubingwa wa ligi kuu soka ya bara.

·      Weekend hii ni patashika nguo kuchanika viwanjani.
·         Patashika hiyo kuanza jumamosi hii na kumalizikia jumapili kwa mechi ya watani wa jadi Simba na Yanga.


                                     Na. Deo kaji Makomba.


Hekaheka za kuwania ubingwa wa ligi kuu soka ya Vodacom Tanzania bara, zinatarajia kuendelea weekend hii huku kukishuhudiwa mechi kadhaa zikipigwa katika viwanja tofauti.

 Timu mbalimbali  zitapambana kuwania pointi tatu muhimu ili kuweza kujiweka kwenye mazingira mazuri katika harakati hizo za kuwania ubingwa wa ligi hiyo ya Tanzania bara.

Jumamosi hii kivumbi cha ligi  Kuu ya Vodacom (VPL) kitaendelea kutimka kwa mechi tano huku Mbeya City ikiikaribisha JKT Ruvu kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya.

Mechi nyingine zitakuwa kati ya Oljoro JKT na Azam (Uwanja wa Sheikh Kaluta Amri Abeid, Arusha), Mtibwa Sugar na Mgambo Shooting (Uwanja wa Manungu, Turiani), Ashanti United na Ruvu Shooting (Azam Complex Chamazi, Dar es Salaam) na Kagera Sugar dhidi ya Coastal Union (Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba).

Licha ya michezo hiyo jumamosi hii, mchezo wa watani wa jadi Simba na Yanga utakaopigwa jumapili hii ndio umekuwa gumzo kubwa miongoni mwa wapenzi na mashabiki wa soka nchini Tanzania, kutokana na timu hizo kuwa na ubipanzani mkubwa pindi zinapokutana uwanjani.


 Picha ikionesha kikosi cha wachezaji wa timu ya Simba cha mwaka wa 2010

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na na nakala yake kukifika kisima chetu cha habari, imeeleza kuwa, Mechi hiyo baina ya Simba na Yanga itaanza majira ya saa 10 kamili jioni.

Ama kwa hakika mchezo huo utakuwa wa vutanikuvute kutokana na kila timu kutaka kushinda mchezo huo ili kujiweka katika mazingira mazuri kwenye msimamo wa ligi kuu hiyo lakini pia kila moja ikitaka kuonyesha utemi kwa mwenzake.

Katika msimu uliopita, wekundu wa Msimbazi Simba walikubali kichapo kutoka kwa watani wao wa jadi Yanga, katika katika mchezo wa marudiano wa ligi hiyo.

No comments:

Post a Comment