Friday 30 August 2013

PILIKAPILIKA NDANI YA JIJI LA MWANZA ZAANZA.



Mwenyekiti wa TCCIA mkoa wa Mwanza, Bw. Elibariki Mmali, akizungumza na wandishi wa habari jijini Mwanza

Ni kutokana na kuanza kwa maonesho makubwa ya biashara ya kimataifa.

·        Makampuni kutoka Kenya, Uganda, Tanzania, China, Misri na Singapore kuonesha bidhaa zao.


·        Mkuu wa mkoa wa Mwanza kuyafungua rasmi septemba 2



 

                                            Na. deo kaji makomba
Maonmesho ya kimataifa ya biashara ya nchi za ukanda wa Afrika mashariki yanaanza ijumaa hii kwenye uwanja mkongwe wa Nyamagana Jijini Mwanza.

Makampuni kutoka nchi za Kenya , Unganda na mwenyeji Tanzania yatashiriki katika maonesho hayo huku nchi za misri, Singapore pamoja na China zikiwa nchi waalikwa kuonesha bidhaa mbalimbali katika maonesho hayo.

Kulingana na taarifa iliyotolewa na chama cha wafanyabiashara mkoani Mwanza, TCCIA, kupitia mwenyekiti wake Bw. Elibariki Mmali, maonesho hayo ijumaa hii na yakitarajiwa kufunguliwa rasmi jumatatu hii septemba 2 mwaka huu na mkuu wa mkoa wa Mwanza, Evarist Ndikilo.

Zaidi ya makampuni 350 kutoka katika nchi za ukanda wa Afrika mashariki pamoja na nchi tatu waalikwa yanatarajia kushiriki maonesho haya ambayo hivi sasa yamefikia mwaka wake wa nane tangu kuanzishwa kwake mnamo mwaka 2005, yakiwa na lengo la kutoa fursa kwa wajasilia mali wadogowadogo katika nchi hizo kuonesha kazi zao wanazozalisha ikiwa ni pamoja na kutanua wigo biashara zao kupitia maonesho hayo.

Akizungumza mbele ya wandishi wa habari jijini Mwanza katika kuelekea kwenye maonesho hayo, mwenyekiti huyo wa TCCIA, mkoani Mwanza, Bw. Mmali, amesema kuwa makampuni ya nje yaliyokuja na bidhaa kwa ajili ya maonesho tu, hayataruhusiwa kuuza bidhaa hizo kwa kuwa zitakuwa zimeletwa kwa ajili ya maonesho.

Tuesday 27 August 2013

MAONESHO YA NANE YA BIASHARA YA KIMATAIFA

Mwenyekiti wa chama cha wafanyabiashara mkoa wa Mwanza, TCCIA, Bw. Elibariki Mmari, akizungumzia mandalizi kuelekea maonesho ya Nane ya biashara kwa nchi za ukanda wa Afrika mashariki, mbele ya wandishi wa habari katika ukumbi wa kipepeo uliopo kwenye hotel ya new Mwanza, juamanne hii



Maonesho ya biashara kwa nchi za Afrika mashariki kufanyika jijini Mwanza.

·        Ni kuanzia Agost 30 mwaka huu.


·        Bidhaa za makampuni mbalimbali kutoka nchi za Afrika mashariki kuwa kivutio katika maonesho hayo.


·        Zaidi ya makampuni 350 kushiriki maonesho hayo.



                         

                                              Na. deo kaji makomba.


Zaidi ya makampuni ya biashara 350 yanatarajia kushiriki katika maonesho ya biashara ya afrika mashariki  yanayotarajia kuanza agost 30 mwaka huu kwenye uwanja mkongwe wa Nyamagana jijini Mwanza.

Makampuni kutoka nchi za ukanda wa afrika mashariki, ikiwemo Kenya, Uganda na mwenyeji Tanzania yatashiriki katika maonesho hayo yaliyofikia mwaka wa nane tangu kuanza kwake, yakiandaliwa  na chama cha wafanyabiashara nchini Tanzania, mkoa wa Mwanza, TCCIA.

Akizungumza na wandishi wa habari katika ukumbi wa kipepeo uliopo kwenye hotel ya New Mwanza, mwenyekiti  wa TCCIA mkoani Mwanza, Bw. Eribaliki Mmari, amesema kuwa licha ya makampuni kutoka ukanda wan chi za afrika mashariki pia makampuni kutoka nchi za China, Misri pamoja na Singapore yatashiriki katika maonesho hayo makubwa.

Kulingana na Bw. Mmari, bidhaa zitakioneshwa  katika maonesho hayo ni bidhaa zitokanazo na kilimo, chakula na vinywaji, viwanda vya nguo, bidhaa zitokanazo na ushonaji pamoja na ufumaji.
 Mwenyekiti wa TCCIA mkoa wa Mwanza, Bw. Mmari, akiwiwa na viongozi wenzake wakati wa mkutano na wandishi wa habari.

Bidhaa zingine zitakazooneshwa katika maonesho hayo ni bidhaa kutoka viwandani pamoja na huduma zitolewazo na makampuni mbalimbali ya mawasiliano na teknolojia nchini Tanzania.

Akizungumzia mafanikio tangu kuanzaishwa kwa maonesho hayo mnamo mwaka 2005, mwenyekiti huyo wa TCCIA mkoani Mwanza, amesema kuwa kumekuwepo na mafanikio makubwa  yaliyopatikana tangu kuanzishwa kwake ikiwemo mafanikio binasfi ya makampuni mbalimbali ambayo yamekuwa yakishiriki katika maonesho hayo, pamoja na serikali kupitia taasisi zake.

Akitolea mfano Bw. Mmari, amesema kuwa maonesho hayo yametoa fursa kwa wawekezaji mbalimbali nchini Tanzania, kuwekeza katika sekta mbalimbali ikiwemo mahotel.
 Picha ikionesha moja ya hotel yenye hadhi ya nyota tano iliyoko katikati ya jiji la Mwanza katika makutano ya barabara za Kenyata na Posta.(Picha zote na deo kaji makomba)

Bw. Mmari ameongeza kusema kuwa maonesho hayo ya biashara kwa nchi za ukanda wa Afrika mashariki yanatoa fursa kwa makampuni yaliyoko nchini Tanzania na jumuiya ya afrika mashariki kuweza kutangaza bidhaa zao.

Maonesho hayo pia yanatarajia kutoa fursa kwa makampuni mbalimbali ya biashara nchini Tanzania kuweza kujifunza na kuongeza uuzaji nje bidhaa kwa ajili ya kuwa tayari kupata faida katika masoko ya kidunia yaliyoandaliwa ikwemo AGOA, EPA, pamoja EBA.



Monday 19 August 2013

MANDAMANO YA CHADEMA “YAINUKISHA” MWANZA.



Askari polisi wakiwa kazini kuwatawanya wafuasi wa CHADEMA
 
Polisi walazimika kutumia mabomu ya machozi kuwatawanya wafuasi wa CHADEMA.

·        Ni baada ya wafuasi wa CHADEMA kukataa kutii amri ya polisi
·        Hali ya hewa yachafuka na shughuli za simama kwa muda jijini Mwanza.
                                    
                              Na. deo kaji makomba.

Polisi mkoani Mwanza wamelazimika kutumia mabomu ya machozi kuwatawanya wafuasi wa chama cha demokrasia na maendeleo, CHADEMA, waliokuwa wamekusanyika katika viwanja vya furahisha jijini Mwanza, kufuatia mandamano ya amani yaliyofanyika jumatatu hii yakianzia katika viwanja vya shule ya msingi Buzuruga  hadi katika viwanja vya furahisha Kirumba.

Mandamano hayo ya wafuasi wa CHADEMA, yaliyoongozwa na mbunge wa Ilemela Bw. Hines Kiwia pamoja na mbunge wa jimbo la Nyamagana Bw. Ezekiel Wenje yalikuwa na lengo la kushinikiza kung’olewa madarakani kwa meya wa manispaa ya Ilmela, Bw. Henry Matata anayedaiwa  kuchaguliwa kinyume cha sheria pamoja na kupinga kufukuzwa kinymela kwa madiwani watatu wa chama hicho.

Madiwani waliofukuzwa na meya wa manispaa ya Ilemela kinyume cha sheria ni Abubakar Kapera diwani wa kata ya Nyamanoro, Marietha Chenyenge(Ilemela) na Dan Kahungu diwani wa kata ya Kirumba jijini Mwanza.
Viongozi wa CHADEMA na wafuasi wao wakiandamana kutoka Buzuruga kuelekea Viwanja vya Furahisha
 
Mandamano hayo yalianza kwa amani na utulivu majira ya saa tano asubuhi, katika viwanja vya hule ya msingi Buzuruga, yakipita katika barabara ya nyerere, Rufiji, balewa na hatimaye kufika katika viwanja vya furahisha huku yakisimamiwa na walinzi wa usalama, jeshi la polisi mkoani Mwanza.

Baada ya kufika katika viwanja vya furahisha uongozi wa CHADEMA, ukiongozwa na Mbunge wa Ilemela, Bw. Hines uliwataka wafuasi wa chama hicho kutulia katika viwanja hivyo vya furahisha kirumba ili wamfuate mkuu wa mkoa wa Mwanza, Evarist Ndikilo, aweze kupokea mandamano hayo.

Lakini baada ya uongozi wa CHADEMA kufika katika ofisi ya mkuu wa mkoa wa Mwanza, walipata fursa ya kuonana na mkuu huyo wa mkoa na kueleza adhima ya mandamano hayo na kwamba kuna taarifa ya kuwepo naarifa kutoka kwa Waziri mkuu na waziri wa serikali za mitaa  TAMISEMI ikiueleza uongozi wa mkuu wa mkoa kuhusiana sakata hilo.
 Picha ikionesha wafuasi wa CHADEMA wakiwa katika viwanja vya furahisha kirumba jijini Mwanza

 Mmoja wa wafuasi wa CHADEMA akionesha msisitizo katika mandamano hayo

 Uongozi huo wa CHADEMA baada ya kufika katika ofisi ya  mkuu wa mkoa Mwanza  ulimtaka kutoa tamko mbele ya wafuasi wa CHADEMA waliokuwa wakisubilia katika viwanja vya Furahisha.

Akizungumza mbele ya wandishi wa habari na uongozi wa CHADEMA ofisini kwake, Bw. Ndikilo alisema kuwa yeye hajapata taarifa yoyote ya kimandishi iliyoandikwa na waziri mkuu ya kuelekeza kuhusiana na suala hilo la kurejeshwa katika uongozi madiwani hao pamoja na sakata la meya Matata, na kuwataka WANACHADEMA, wasifanyie kazi taarifa ambazo haziko katika mandishi.
Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama, mkuu wa mkoa wa Mwanza, Evarist Ndikilo akiongea na viongozi wa CHADEMA ofisini kwake
 Viongozi wa CHADEMA wakiwa wamewasili kwenye viwanja vya furahisha

Aidha Bw. Ndikilo aliwashauri viongozi hao wa CHADEMA, akiwemo mbunge wa ilemela Bw. Hines kwa pamoja na mkuu wa mkoa na mbunge wa Ilemela waende katika ofisi waziri wa wizara husika ili kulifuatilia suala hilo.

Lakini wakati mjadala huo ukiendelea huku nyuma wafuasi wa CHADEMA, waliokuwa katika viwanja vya Furahisha waliamua kwenda kwenye ofisi ya mkoa na ndipo polisi walipowazuia wafuasi hao na kuwataka watawanyike lakini wafuasi wa CHADEMA hawakukubaliana na kauli hiyo huku wakitaka kuelekea katika ofisi ya mkuu wa mkoa na ndipo mambo yalipobadilika kwa kwa polisi kutumia mabomu ya machozi ili kuwatawanya wafuasi hao.
Tayari kimeanza kimeanza "kunuka"
Polisi wakizima moto uliokuwa umewashwa na wafuasi wa CHADEMA
Barabara ikiwa imewekewa vizuizi wakati wa vurugu hizo jijini Mwanza
Polisi wakiwa kazini
Kama kawaida kazini polisi wakifanya yao
Mama huyu ni miongoni mwa wafuasi wa CHADEMA, aliyejitokeza katika mandamano hayo yaliyokuwa na lengo la kushikiza meya wa Halmashauri ya Ilemela Bw. Matata aondolewe madarakani(Picha na Deo Kaji Makomba)

Saturday 17 August 2013

MASHINDANO YA ALLIANCE SCHOOL EAST AFRIKA TOURNAMENT.

 Mkurugenzi wa Alliance academy school ya jijini Mwanza, James Bwire, wakati akizungumza na Kisima hiki cha habari.(Picha na Deo Kaji Makomba)


Mashindano ya soka kwa vijana wa Afrika Mashaririki



·       Kuanza kurindima jumapili hii uwanja wa Nyamagana


·       Timu kutoka ukanda wa Afrika mashariki na kati kushiriki mashindano hayo.



                                  

                                      Na. deo kaji makomba.

Mashindano ya soka maarufu kama Alliance school Mwanza east Afrika tournament, yanatarajia kuanza jumapili hii agost 18 mwaka huu kwenye uwanja mkongwe wa Nyamaganaga jijini Mwanza.

Mashindano hayo ya soka yatakayoshirikisha timu za shule za michezo kutoka katika ukanda wa Afrika mashariki na kati yamendaliwa na shule ya Alliance academy iliyopo kata ya Mahina jijini Mwanza.

Kulingana na uongozi mkuu wa wa Alliance academy, shule kutoka Kenya, Uganda, Burundi, Rwanda, jamuhuri ya kidemocrasia ya Congo pamoja na wenyeji Tanzania zitashiriki katika mashindano hayo yenye lengo la kuwapatia ushindani wachezaji kutoka katika shule ya alliance, lakini pia kujenga mahusiano mazuri miongoni mwa nchi washiriki katika mashindano hayo.

Akizungumza na Kisima chetu cha habari ofisini kwake jijini Mwanza, mkurugenzi wa shule ya Alliance academy, James Bwire, amesema kuwa, jumla ya timu 27 kutoka katika nchi za ukanda huo wa Afrika mashariki na kati zitashiriki katika mashindano hayo.
 Timu ya Alliance academy ikiwa katika mazoezi kujiandaa na mashindano hayo ya Afrika mashariki na kati.

Aidha Bw. Bwire ameongeza kusema kuwa mandalizi yote kuelekea mashindano hayo yamekwishakamilika na kwamba jumapili hii mashindano hayo yataanza kurindima kwenye uwanja mkongwe wa Nyamagana, jijini Mwanza.

Katika mahojiano yake na Kisima cha habari, Bwire ameongeza kusema kuwa milango iko wazi kwa wale wote wenye mapenzi mema kuweza kufadhili mashindano hayo yenye lengo la kuendeleza vipaji vya soka la vijana wa Tanzania ili kuwaweza siku za usoni kuweza kujiali kupitia michezo ikiwemo soka.

Mashindano hayo yanatarajia kufikia tamati hapo Agost 20 mwaka huu.