Monday 12 October 2015

WAZIRI KIGODA HATUKO NAYE TENA






                        Aliyekuwa waziri wa viwanda na biashara Abdalah Kigoda

WAZIRI KIGODA AFARIKI DUNIA HUKO INDIA.

Waziri wa Viwanda na Biashara Dk. Abdallah Kigoda amefariki dunia leo saa 10 jioni nchini India alipokuwa amelazwa akipatiwa matibabu.

Katibu wa Bunge Dkt Thomas Kashilila amethibitisha taarifa hizo, na kusema kuwa Dkt Kigoda alikuwa akitibiwa katika hospitali ya Apollo, New Delhi na kwamba taarifa zaidi zitatolewa baadaye.

Kwa mujibu wa kaka wa marehem Sadiki Kigoda aliyezungumza na na vyombo vya habari siku chache zilizopita, alisema kuwa Dkt Kigoda alikuwa akisumbuliwa na matatizo ya figo kushindwa kufanya kazi.


 

STARS HIYOOO!

 
      Kikosi cha timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa stars, kilichopambana huko Malawi

HEKA HEKA ZA KUWANIA KUPANGWA KWENYE MAKUNDI YA TIKETI ZA FAINALI ZA KOMBE LA DUNIA.
  •     Licha ya kufungwa bao 1-0 na Malawi, Stars yafuzu hatua ya pili 
                                  Na. Mwandishi wetu

Tanzania imeweza kutimiza ndoto za kutinga hatua ya mwisho ya mchujo kuwania kupangwa kwenye makundi ya kuwania tiketi ya Fainali za Kombe la Dunia, licha ya kufungwa 1-0 na Malawi jumapili iliyopita, katika Uwanja wa Kamuzu mjini Blantyre.

Tanzania inasonga mbele kwa ushindi wa jumla wa 2-1, baada ya Jumatano iliyopita kushinda 2-0 Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam katika mchezo wa kwanza wa hatua ya kwanza ya mchujo.

Katika mchezo huo uliochezeshwa na refa wa Angola, Martins de Carlvalho aliyesaidiwa na Gadzikwa Bongani wa Zimbabwe na Valdmiro Ntyamba wa Angola, hadi mapumziko Malawi walikuwa mbele kwa bao hilo 1-0, lilifungwa na John Banda dakika ya 42 aliyefumua shuti kali akimalizia pasi ya Chiukepo Msowoya.

Taifa Stars ndio walioanza mchezo huo kwa kasi na dakika ya kwanza tu, mshambuliaji Mbwana Samatta alikaribia kufunga, baada ya kumtoka beki Limbikani Mnzava, lakini kipa Simplex Nthala akaokoa.

Malawi wakajibu shambulizi dakika ya pili baada ya shuti kali la Banda kupanguliwa na kipa Ally Mustafa ‘Barthez’. Barthez akafanya kazi nzuri tena dakika ya 10 baada ya kuokoa michomo miwili mfululizo ya Malawi.

Stars ilizinduka dakika ya 35 baada ya Thomas Ulimwengu kumtoka vizuri beki wa Malawi Yamikani Fodya baada ya pasi ndefu ya Samatta, lakini shuti lake likaenda nje sentimita chache.
Kipindi cha pili, kocha wa Stars, Charles Boniface Mkwasa alianza na mabadiliko, akimtoa kiungo Said Ndemla na kumuingiza mshambuliaji John Bocco.

Mabadiliko hayo yaliifanya Stars ianze kudumu kwenye eneo la Malawi, lakini bado mashambulizi ya hatari yalielekezwa langoni mwa Tanzania.

Dakika ya 58 Nahodha wa Tanzania, Nadir Haroub ‘Cannavaro’ aliokoa hatari langoni mwake na dakika ya 62 Malawi walifanya mashambulizi matatu mfululizo ya hatari lanoni mwa Stars, ikiwemo kupata kona mbili.

Dakika ya 72 Mbwana Samatta alipiga shuti hafifu akiwa karibu na lango baada ya kupokea pasi nzuri ya John Bocco likaenda nje.

Malawi walifanya shambulizi la hatari dakika ya 90, lakini Robin Ngalande akashindwa kumalizia vizuri baada ya kupiga nje.
Kwa matokeo hayo, Taifa Stars sasa itamenyana na Algeria katika mechi za mwisho za mchujo mwezi Novemba.

Kikosi cha Tanzania; Ally Mustafa ‘Barthez’, Shomary Kapombe, Mwinyi Hajji, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Kevin Yondan, Himid Mao, Thomas Ulimwengu, Said Ndemla/John Bocco dk46, Mudathir Yahya, Mbwana Samatta na Farid Mussa/Mrisho Ngassa dk75.

Malawi; Simplex Nthala, Stanley Sanudi, Miracle Gabeya/Robin Ngalande dk76, Yamkani Fadya, Limbikani Mzava, Gerald Phiri, Chimango Kayira, Micium Mhone, Chiukepo Msowoya, John Banda na Shumaker Kuwali.

Thursday 10 September 2015

AZAM, TFF ZARUDISHA KOMBE LA SHIRIKISHO

 
Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF) kwa udhamini wa kampuni ya Azam Media kupitia Azamtv Sports leo wamezindua kombe la Shirikisho litakalofahamika kama Azam Sports Federation Cup (ASFC) ambalo litaanza kutimua vumbi mwezi Novemba mwaka huu kwa kushirikisha timu 64 nchini.
Kurudishwa kwa michuano hii imekua ni faraja kwa wapenzi na wadau wa mpira miguu nchini baada ya kukosekana kwa takribani miaka 13 michuano hiyo, ambapo sasa Bingwa wa kombe la Shirikisho ataiwakilisha nchi katika michuano ya Kombe la Shirikisho Barani Afrika (CAFCC).

Akiongea na waandishi wa habari wakati wa uzindizi wa michuano hiyo na kuchezeshwa droo ya awali, Rais wa TFF Jamal Malinzi amemshukuru Mkurugenzi wa Azam Media Rhys Thorrington kwa kuweza kudhamini michuano ambayo itongeza ushindani zaidi nchini.

Malinzi amesema anaviomba vilabu vitakavyoshiriki michuano ya kombe la hilo, vionyeshe ushindani mkubwa kwani ndio nafasi pekee ya kuweza kuitangaza na kuonekana kwa kuwa michuano hiyo itakua ikionyeshwa moja moja na luninga ya Azamtv.

Aidha Malinzi amesema kila timu inayoshiriki michuano hiyo itapata fedha ya usafiri shilingi milioni 3, na vifaa vitakavyotolewa na mdhamini kampuni ya Azam Media.

Naye Mkurugenzi wa Azam media Rhys Thorrington amesema uhdmaini huo wa miaka mine una thamani ya fedha za kitanzania bilioni 3.3  ambapo timu zitakazoshiriki michuano hiyo zitapata nafasi ya kuonekana moja moja katika nchi zaidi ya saba barani Afrika kupitia kituo chao cha azamtv.
Mshindi wa Kombe la ASFC linalodhaminiwa na kampuni ya Azam kupitia Azamtv Sports, atajinyakuliwa kitita cha shilingi milioni hamsini (TZS 50,000,000), jumla ya timu 64 kutoka Ligi Kuu (VPL), ligi daraja la kwanza (FDL) na ligi daraja la pili (SDL) zitashirki katika kombe hilo.TFF President, Jamal Malinzi and Azam Media CEO Rhys Thorrington
 Jamal Malinzi, Rhys Thorrington

Timu zote 24 za ligi daraja la pili na 8 za ligi daraja la kwanza 3, zilizopanda daraja na 5 zilizoshika nafasi za chini kwenye makundi yote zitashiriki katika raundi ya kwanzamwezi Novemba kwa kucheza mechi 16 na kupata washindi 16 ambao wataingia raundi ya pili.

Timu 16 zilizoshinda raundi ya kwanza na 16 zilizofanya vizuri ligi daraja la kwanza zitachanganywa na kupangwa kucheza mechi 16 nyingine za raundi ya pili mwezi Desemba.

Washindi wa raundi ya pili wataingia raundi ya tatu ambapo watachanganywa na timu 16 zilizopo ligi kuu na kuchezwa mechi 16 nyingine ambazo washindi wake wataingia raundi ya nne. Raundi hii ya tatu itafanyika mwezi Januari 2016.

Timu 16 zilizoshinda raundi ya tatu zitaingia raundi ya nne zitapangwa ili kucheza hatua hii ambayo itakuwa na mechi  8 na washindi 8 wataingia katika hatua inayofuata ambayo ni raundi ya tano au robo fainali. Raundi hii ya nne itachezwa Februari 2016.

Washindi wa raundi ya nne watapata nafasi ya kuingia raundi ya 5 ambayo pia ni robo fainali, droo itapangwa. Raundi hii ya tano itachezwa mwezi Machi 2016.
Washindi wa raundi ya tano au robo fainali watapangwa kucheza nusu fainali au raundi ya 6 mwezi Aprili.

Washindi wa nusu fainali watapambana katika fainali na kumpata bingwa wa Azam Sports Federation Cup 2015/16. Mechi ya fainali itachezwa wiki moja baada ya ligi kuu kumalizika na Bingwa atakabidhiwa kombe na zawadi ya fedha tasilimu shilingi milioni 50.

Mechi za raundi ya kwanza na raundi ya pili kama mshindi hatapatikana ndani ya dakika 90 basi mshindi atapatikana kwa kupigiana penati moja kwa moja. Mechi za raundi ya tatu na nne kama mshindi hatapatikana ndani ya dakika 90 mechi itarudiwa katika uwanja wa timu iliyokuwa mgeni mechi ya awali.

Mechi za robo fainali au raundi ya tano kama mshindi hatapatikana ndani ya dakika 90 hatua ya penati tano tano itaamua mshindi.

Kwa mechi za nusu fainali na fainali kama mechi itaisha kwa sare ndani ya dakika 90, dakika 30 za nyongeza zitachezwa, na kama hakutakuwa na mshindi penati zitaamua mshindi.

Raatiba ya raundi ya kwanza:
AFC -Arusha Vs Polisi Mara, Polisi -Tabora Vs Green Worries -Dar es salaam, Karikoo Lindi Vs Changanyikeni -Dar es salaam, Mkamba Rangers –Morogoro Vs Mvuvuma - Kigoma, Rhino Tabora Vs Allicane - Mwanza, Panone Kilimanjaro Vs Coca Cola Mbeya, Polisi Morogoro Vs Mshikamo Dar es salaam, Sabasaba Morogoro Vs Abajalo Tabora.

Magereza Iringa Vs Polisi Dar es salaam, Milambo Tabora Vs Town Small Ruvuma, Abajalo Dar es salaam Vs Transit Camp Dar es salaam, Ruvu Shooting Vs Cosmopolitan Dar es salaam, JKT Rwamkoma Mara Vs Villa Sqaud (Dar es salaam), Wenda FC Mbeya Vs Madini Arusha, Pamba FC Mwanza Vs Polisi Dom, Singida United Vs Bulyanhulu FC Shinyanga

Wednesday 9 September 2015

WATUKUTU WA STAND CHAMA LA WANA WAULA


Description: Description: cid:image001.jpg@01D0E7B4.C93E0980

Mwenyekiti wa stand united Amani Vicent (kushoto) akibadilishana mkataba wa udhamini wa timu hiyo na Makamu wa rais wa ACACIA anaeshugulikia masuala ya Kampuni, Deo Mwanyika mara baada ya kutiliana saini mkataba wa miaka miwili na kampuni hiyo.
 

ACACIA YAIDHAMINI TIMU YA STEND UNITED KWA BILIONI MOJA

·        Ni udhamini mnono wa miaka miwili.
·        Udhamini huo umelenga kukuza soka kwa vijana.

Ijumaa, Septemba, 4th 2015: Kampuni ya uchimbaji wa madini ya dhahabu ya Acacia iliingia mkataba wa miaka miwili na timu ya Stend United ya Mkoani Shinyanga kwa ajili ya kushiriki ligi kuu ya Vodacom ambayo inategemewa kuanza tutimua vumbi katikati ya mwezi huu. Stand United ni moja kati ya timu bora kabisa katika kanda ya ziwa ambayo imeshiriki katika ligi kuu msimu uliopita 2014/2015 na kumaliza ikiwa nafasi ya tisa.

Udhamini wa ACACIA katika misimu hii miwili ya ligi kuu itasaidia katika kuifanya timu ya Stand United iweze kufanya vizuri katika michezo yake, pamoja na kusaidia katika kuboresha programu mbalimbali za timu na kuendeleza vipaji pamoja na masuala ya Utawala.
 Description: Description: cid:image002.jpg@01D0E7B4.C93E0980
Aman Vincet, mwenyekiti wa timu ya Stand United kushoto na Deo Mwanyika kulia ambaye ni makamo wa rais wa uendeshaji wa shughuli wa kampuni ya Acacia, wakionesha mkataba mbele ya wageni waalikwa katika hafla fupi ya kutiliana saini kuidhamini timu yake katika hotel ya Vigmark mjini shinyanga.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo Makamu wa rais wa Acacia aneshughulikia masuala ya kampuni, Deo Mwanyika, amesema  “Kwa takriban mwaka mmoja, tumekua tukifanya kazi pamoja na Stand United. Kwa muda huo tulianzisha mchakato wa kutambua namna nzuri ya kuboresha ushirikiano wetu ili kunufaisha watu wa Shinyanga na Kanda ya Ziwa kwa ujumla.

Bwana Deo amesema Msimu uliopita uliwapatia fursa nzuri ya kushuhudia uwezo wa timu hiyo hasa ukizingatia ilikua mara yao ya kwanza kushiriki ligi kuu, “Baada ya tathmini ya kina, tunadhani huu ni muda muafaka wa sisi kusaini makubaliano au mkataba wa kuidhamini na kufanya kazi pamoja ya kuikuza timu hii ya nyumbani maarufu kama “Chama la wana”.
 Description: Description: cid:image003.jpg@01D0E7B4.C93E0980
 Baadhi ya wachezaji wa Stend United wakionyesha jezi watakazotumia msimu huu wa ligi kuu ya Vodacom mara baada ya kukabidhiwa vifaa mbalimbali na wadhamini wao kampuni ya ACACIA. Kutoka kushoto ni Seleman Mrisho, Frank Hamis,Shabani Dunia, Geremia Enos, Jonh Mwenda na Kheri Khalfan

Hivyo, Leo, Acacia tunasaini mkataba na timu ya Stand United kwa udhamini wa misimu miwili ya ligi kuu, wenye thamani ya Shilingi bilioni moja. Udhamini huu unajuamuisha shughuli za uendeshaji wa timu, kuboresha uongozi na kukuza vipaji.
 Description: cid:image037.jpg@01D0E7DF.5D38C830
 Wachezaji wa Stend United wakionyesha jezi yao itakayokuwa ikitumika kwa michezo ya uwanja wa nyumbani na ile ya ugenini wakati wa msimu wa ligi kuu ya Vodacom.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Stand United Amani Vincent, amesema udhamini huo wa miaka miwili utakuwa chachu kwa timu yake kufanya vizuri katika ligi kuu, “Msimu uliopita tulimaliza tukiwa nafasi ya nane na kipindi hicho hatukuwa na fedha ya kutosha kuendesha timu, lakini kwa udhamini tulioupata kutoka kwa ndugu zetu wa Acacia vijana wetu safari hii watafanya vizuri zaidi.
 Description: cid:image039.jpg@01D0E7DF.5D38C830

 Description: cid:image041.jpg@01D0E7DF.5D38C830
 Mkuu wa mkoa wa Shinyanga, Ali Nassoro Lufunga akikabidhiwa jezi na makamo wa rais wa Acacia Deo Mwanyika, kabla ya kuanza kwa mechi kati ya Stand United na Olympic Stars ya Burundi kwenye uwanja wa CCM Kambarage mjini Shinyanga.

Description: cid:image042.jpg@01D0E7DF.5D38C830
 Kikosi cha Acacia Stand United, kikipasha moto misuli kabla ya mechi dhidi ya Olympic Stars, ambapo Acacia Stand United chama la wana waliibuka washindi kwa bao 1-0
 Description: cid:image032.jpg@01D0E7DF.5D38C830
 Baadhi ya washabiki wa Stend United waliohudhuria wakati wa uzinduzi wa jezi mpya za timu hiyo ikiwa pia ni sehemu ya kusherekea udhamini wao na kampuni ya Uchimbaji wa madini ya ACACIA.

Kampuni ya Acacia ni kampuni inayoongoza kwa shughuli za uchimbaji wa madini hapa Tanzania huku ikiwa na Migodi mitatu katika kanda ya ziwa, kupitia mradi wa “Acacia Maendeleo Fund” ambao ndio pia umetoa udhamini wa timu ya Stend umekuwa pia ukitekeleza miradi mbalimbali ya Maendeleo kwa Jamii hapa nchi huku kampuni hiyo ikieleza kuwa dhamira yake ni kuendelea kufanya kazi na Jamii zinazowazunguka katika kuwaletea Maendeleo wenyeji.